Utoshefu Lyrics
- Genre:Bongo Flava
- Year of Release:2021
Lyrics
Utoshefu - Ambwene Mwasongwe
...
Nime jifunza kuwa radhi
Katika hali yoyote niliyo nayo
Najua kudhiliwa, tena na kufanikiwa
Katika hali yoyote
Na Katika mambo yoyote
Nimejifunza kushiba
Na kuona njaa
Nimejifunza kuwa na vingi
Na kupungukiwa
Nayaweza yote kwa anitiaye nguvu
Utauwa na kuridhika vimenipa utoshefu
***
Furahini siku zote katika Bwana
Anasema ndugu zangu Furahini
Upole wenu ujulikane na watu wote
Bwana yu karibu Kuja
Furaha niliyonayo ni tunda la Roho
Furaha Hiyo hailetwi na vitu
Sisubiri nipewe ili nifurahi
Nafurahi hata kwenye mateso
Upole nilionao umetoka kwa Roho
Hautegemei ninavyotendewa
Amani ya KRISTO imenitawala ndani
Naimba wimbo wakati wa shida
Imenihifadhi moyo na Nia yangu
Ninayapenda mambo ya staha
Haki, usafi, kupendeza na sifa njema
Ukiwepo wema wowote nautafakari
Nafurahi nimehuishwa fikra zangu
Nafurahi nimeridhika na Utauwa wa Bwana
"" "" ""
Upendo wa Dunia hii una sababu
Sababu hizo zikiisha huisha
Upendo huo ni wa nipe nikupe
Vitu vikienda na upendo umeenda
Furaha ya Dunia hii ni ya sababu
Ukivikosa vitu inaisha
Amani ya Dunia hii ni ya sababu
Hutengenezwa na mazingira yasiyodumu
Naupenda
Utauwa(niliopokea kutoka kwa Bwana) na kuridhika vimenipa utoshefu
(Naupenda) Utauwa (na sifa njema) na kuridhika vimenipa utoshefu
Utauwa na kuridhika vimenipa utoshefu
Ooo!
"" ""
Nitawapenda watu tena nitawaamini
Nitakupenda zaidi wewe usiyeumiza
Nitafurahi tena nitatabasamu na kuonyesha
Mwanya, ila sitawapa moyo
Moyo hudanganya
Nitaukabidhi kukupa wewe uliyeuumba
Moyo huua
Sitampa mtu maana haujui
Watu wanatibu ila wewe waponya
Wao hunenepesha ila wewe unawandawisha
Japo twaanguka twaumia twateseka
Tunalia
Wewe Bwana ni Faraja yetu
Nimeridhika na Utauwa umenipa kutosheka
Nimeridhika nimekupa moyo wangu uutawale
(Katika jumla ya yote)
Nime jifunza kuwa radhi
Katika hali yoyote nilivyo nayo
Najua kudhiliwa, tena na kufanikiwa
Katika hali yoyote
Na Katika mambo yoyote
Nimejifunza kushiba
Na kuona njaa
Nimejifunza kuwa na vingi
Na kupungukiwa
Nayaweza yote kwa anitiaye nguvu
Nime jifunza kuwa radhi
Katika hali yoyote nilivyo nayo
Najua kudhiliwa, tena na kufanikiwa
Katika hali yoyote
Na Katika mambo yoyote
Nimejifunza kushiba
Na kuona njaa
Nimejifunza kuwa na vingi
Na kupungukiwa
Nayaweza yote kwa anitiaye nguvu
Nime jifunza