Nguvu ya kujua Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2021
Lyrics
Nguvu ya kujua - Ambwene Mwasongwe
...
Namjua Mungu
(Namjua Bwana)
Namjua
Namjua Mungu
(Namjua yeye)
Namjua
Alionekana sura yake kama malaika
Moyo mweupe uliotulia akiwaza mema
Ukimtazama Alivyopendeza anavutia
Tabasamu lake hata mbinguni walilikubali
Kama pilipili iliyotiwa kidondani na mkorofi
Ndivyo furaha yake ilivyoondolewa na jambo dogo
Kama pilipili iliyotiwa kidondani na mkorofi
Ndivyo Amani yake ilivyoyeyushwa na jambo dogo
Nikaukumbuka uongo wa shetani kumdanganya Eva
Ukifanya hivi utayajua mema na mabaya
Wakajisahau mema tayari waliyajua
Nia ya shetani 'litaka wajue mabaya
Nguvu ya kujua mabaya Kuna madhara mengi
Ni kheri moyo wako ungejazwa na mambo mema
Alipojua amepata kansa kafa mapema (hakuishi )
Alipojua amesalitiwa akazimia
Alipojua kafukuzwa kazi kachanganyikiwa
Angemjua Mungu angepata neema ya kumsaidia
"" "" ""
Moyo wa mtu ni kichaka umehifadhi mambo mengi
Uchungu, wivu na husuda na dhambi na mabaya mengi
Mungu alipoumba mtu alitaka ajue mema tu
Hakuthubutu kabisa ajue na mabaya
Nguvu ya kufa mtu imebebwa kwenye ubaya
Mkila tunda hili mtajua mema na mabaya
Mkila tunda hili mavumbini mtarudi
Lilikuwa ni tunda lenye kujua mema na mabaya
Mema walisha kuwa nayo
Mungu hakuwa na shida
Shetani alichokifanya kuhakikisha wajue ubaya
Hapo kikawa chanzo cha kifo.
Kikawa chanzo cha magonjwa
Kikawa chanzo cha kilio
Kikawa chanzo cha maumivu
Namjua Mungu
Namjua
(Yeye ni chanzo cha Amani)
Namjua Mungu
(Yeye ni mwaminifu )
Namjua
"" ""
Nguvu ya kujua mabaya Kuna madhara mengi
Ni kheri moyo wako ungejazwa na mambo mema
Alipojua amepata kansa kafa mapema
Alipojua amesalitiwa akazimia
Alipojua kafukuzwa kazi kachanganyikiwa
Angemjua Mungu angepata neema ya kumsaidia
Nguvu ya kujua mabaya Kuna madhara mengi
Ni kheri moyo wako ungejazwa na mambo mema
Alipojua amepata kansa kafa mapema
Alipojua amesalitiwa akazimia
Alipojua kafukuzwa kazi kachanganyikiwa
Angemjua Mungu angepata Neema ya kumsaidia
"" "" "