Moyo Wa Ibada Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2021
Lyrics
Moyo Wa Ibada - Ambwene Mwasongwe
...
Wengi wamekusifia
Wengi wamekuimbia
Wengi wamekutolea Bwana
Sadaka na maombi mazuri
Na ibada
Natamani nikusifu
Natamani nikuimbie
Nataka nikutolee
Ibada, sadaka na maombi hujawahi kuyasikia
Ila maneno yananipelea
Na matendo yananikosa
Yamepimwa kwenye mizani
Yameonekana ni mepesi
Mawazo yangu hayatoshi
Fikra zangu ni laini
Hata niweze kukusifu
Uketiye patakatifu
Sasa naomba, maneno
Na Mawazo ya moyo wangu
Yapate kibali mbele zako
Kweli wewe ni Mungu
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Wewe ni mtakatifu)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Jina lako mkweli )
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Hakuna kama wewe)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Matendo yako ni Makubwa Bwana )
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Shuhuda zako hazina maswali)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(wewe ni mtakatifu)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Hakuna kama wewe Bwana )
Ni wewe
Ni wewe Bwana
"" "" ""
Nimeshindwa kuhesabu
Ulofanya kwangu hayahesabiki
Hakuna namna yoyote inayoweza
kupima wema wako kwangu
Nimetafuta kitu gani
Nilichoanza kukupa
Ili unirudishie
Nimegundua nilivyonavyo vyote
Wewe Mungu ndiwe ulianza kunipa kwanza
Nikurudishie nini
Kwa ukarimu ulonitendea
Nime jaribu kufanya vizuri
Ili yamkini niwazidi wote
Ila, nimetafuta sadaka nzuri nitoe
Ibrahimu ameniwahi
Nimetafuta moyo mzuri wa upole
Moyo wa Musa umenishinda
Nime tafuta staili nzuri nicheze
Daudi kacheza zote
Sasa naomba maneno
na mawazo ya moyo wangu
Yapate kibali mbele zako
"" "" "" "" ""
Sasa nimeshasogea
Kwenye vilindi vya moyo wa ibada
Huko yanakosikika
Maneno haijuzu mwanadamu kuyanena
Ila ninatetemeka maana kiti chako
Kina utukufu mwingi
Na tena Jina lako
Unaitwa Mungu wa yasiyo wezekana
Wewe waweza chota maji kwa wavu
Tena waweza kuhifadhi giza nuruni
Wewe waweza kupanda mlima
kwa baiskeli isiyo na mnyororo
Wewe waweza piga mluzi
Huku umefumba maji mdomoni
Wewe waweza vunja jiwe kwa yai
Waweza nasa chuma kwa kijiti
Napata ugumu wa kukusifu Bwana
Maana sifa hizi unazijua zote
Sasa naomba maneno
na mawazo ya moyo wangu
Yapate kibali mbele zako
Kweli wewe ni Mungu
Ni wewe (Hilo ndilo Jina lako)
Ni wewe Bwana
(Hizo ndizo sifa zako)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(wewe mfalme wa wafalme)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Matendo yako ni makubwa)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Shuhuda zako hazina maswali)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Wewe ni mtakatifu)
Ni wewe
Ni wewe Bwana
(Hakuna kama wewe Bwana )
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Ni wewe Bwana
*