Misuli Ya Imani Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2014
Lyrics
Misuli Ya Imani - Ambwene Mwasongwe
...
Ninamkumbuka mama mmoja
Aliyekuwa na Watoto saba
Alikuwa akimcha Mungu
Akimwomba mchana na Usiku
Ulipita muda sijaonana naye
Nikaamua niende nimtembelee
Nikamkuta mama mjane amechoka
Macho yamevimba kwa kulia
Akanitazama akaniambia
Ajali imeua watoto wangu
Tazama kaburi kama matuta
Mungu hakunisazia kitu
Akanikumbusha unajua mwanangu
Wewe bado ni kijana mdogo
Usijefikiri kumwacha Mungu
Hata kama amekuumiza
Akapiga magoti akitetemeka
Akamuomba Mungu mbele yangu akisema
Kwanini uliamua kuchukua wangu tu!?
(Ee Bwana)
Mtaa mzima hukuona wengine!?
(Bwana!)
Kwa nini Ajali moja iliua wangu tu!?
(Kwanini Bwana)
Kwanini siku moja walizikwa wangu tu
(Bwana)
Kwanini huku amua hapa mtaani,
(Nauliza Bwana)
Angalau kila nyumba angekufa
mmojammoja
(Bwana)
Hata nijulize maswali mengi
(Bado wewe Bwana)
Jibu bado litabaki wewe ni Mungu tu
Najua uliniamini hili naliweza
Hivyo basi Nasema Jina lako libarikiwe Amen.
"" "" "" "" ""
Kama kawaida wanadamu
Wakanyanyua vinywa wakasema
Kila mmoja aliongea lake
Ilimradi wamvunje moyo
Wako walojifanya kuwa wana uchungu
Kumbe moyoni wa ng'ong'a
Wengine wakadiriki kusema hadharani
Alijivuna sasa kiko wapi
Mama anasema akiwa msibani
Alihisi mwili unawaka moto
Aliona kama Mungu hayupo
Dunia yote kaachwa peke yake
Waliomfariji aliwaona waongo
Hawajui uchungu wa msiba
Huzuni ilipozidi akalia sana
Asikubali kufarijiwa
Ghafla akakumbuka mtetezi wake
Kwamba Mungu wake yuko hai
Akiisha mpitisha kwenye tanuru
Mwisho atang'ara kama dhahabu
(Hee Bwana)
Ulipomchukua mume wangu Bwana
Watoto walinifariji
(Sasa Bwana)
Sasa umeamua kuwachukua wote
(Wala)
Hakunisazia kitu
(Umenibebesha)
Umenibebesha mzigo mzito sana
(Mimi Bwana)
Siuwezi peke yangu
(Bwana Bwana)
Bila msaada wako
Sitaweza mimi(Ee Bwana) naomba nisaidie
(Haleluya )
"" "" "" ""
Kama unadhanj la kwako zito
Basi sasa jifunze kwa wenzako
Maana wewe kuguswa tu na tatizo
Unanung'unika Mwaka mzima
Waweza kudhani kwamba unaumwa
Kumbe hujaona wagonjwa
Ukishawaona wagonjwa wenyewe
Unaweza kupona bila dawa
Mungu Anao watu anaowaamini
Watu Wenye misuli ya Imani
Wao Wanapopita kwenye magumu
Wanamtukuza katika hayo
Hawa ndio watu Mungu huwatumia
Kumsimangia shetani
Maana kujaribiwa kwa Imani zao
Huleta utukufu kwa Mungu
Mama anasema Mungu ni mwema
Kwa sababu amenitetea
Katika kupitia kwenye magumu
Nimeona mkono wa neema
(Haleluya)
Ashukuriwe Mungu wa watakatifu
(Mungu wa Ibrahimu)
Anayetupa kushinda
(Hata tukipita)
Hata tukipita kwenye magumu gani
(Yeye Bwana)
Hatatuacha peke yetu
(Ameahidi Yesu )
Ametuahidi atakuwa nasi
Hadi ukamilifu wa dahari ee
**HALELUYA!! **