Kuaminiwa Na Mungu Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2014
Lyrics
Kuaminiwa Na Mungu - Ambwene Mwasongwe
...
Huuuuu, yeahyeahyaa
Na kumbuka nikiwa mdogo
Mimi na ndugu zangu
Siku moja tulikaa mezani
Tulitembelewa na mgeni
Mwenye Rika kama yetu
Akaambiwa aombee chakula
Aliomba maombi mazuri
Sote tulifurahia
Sio kwamba tulikuwa hatuombi
Tulifundishwa kuomba
Japo tuliomba kwa kukariri
Wazazi wetu waliposikia
Waliyapenda maombi yale
Wakatunong'oneza wanawe
Tunataka nanyi muokoke
Muombe kama hivi
(Kwa wakati huo) Hatukujua nini maana yake
(Labda kwa kuwa) Labda kwa kuwa(kwa Kweli tulikuwa ) tulikuwa wadogo
(Ila Mungu) Kumbe Mungu(Mungu mbinguni) anafuatilia
Aliiona shauku(ya baba na Mama) ya wazazi
Leo hii tumeshaokoka
***
Nikikumbuka huwa nacheka
Wakati mwingine nalia
Njia yangu haikuwa rahisi
Nilisoma sana Neno la Mungu
Nikajitazama nilivyo
Nikajihurumia mwenyewe
Yako wapi matendo ya Mungu
Yaliyohadithiwa humu
Kwa huzuni nikaamua kufunga
Ili nimueleze
Nataka kujihuzulu huduma
Kwani majaribu kwangu hayaishi
Na ninazidi kuchakaa
Ni Bora uwape watu wengine
Mzigo huu ni mzito kwangu
Kwanza mimi ni mdogo
(Ambwene ) Je unam(Ambwene mwanangu) gomea Nani!?
(Hivi hujajua tu!?) Nimekupa(Ambwene mwanangu) kazi ya kufanya
(Hebu songa mbele) Ukishinda utavikwa taji
(Hivi hujui?) Majaribu kwako ni mtaji
(Ambwene mwanangu) Hebu songa mbele
***
Sasa nimejua siri za Mungu vile anavyotujali
Yeye huona tusivyoviona
Huviona vikwazo vilivyo mbele hapendi tuangamie
Ndio maana hutuandaa mapema
Tungefukuzaje maadui elfu
Bila kuanza na mmoja
Yeye ashikapo kipimo chake apate kutujaribu
Kigezo chake ni uaminifu
Hutumia mambo madogomadogo
Tuyaonayo halali
Ili kupima uaminifu wetu
Angetuwekaje kwenye mambo makubwa
Ikiwa madogo hatuwezi
(Nimegundua) Ni jambo moja kumwamini Mungu
(Ni kitu kingine) Yeye kukuamini
Mpaka akuite rafiki yake
Akuoneshe mbele za shetani
Akuoneshe(Kama Ayubu) mbele za shetani
Yahitaji uaminifu
Nilitiwa moyo na haya yote
Nikamwadhimisha yeye
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe
Uliyefanya haya yote
Ni wewe
Uliyeniokoa mimi
Ni wewe
Ni wewe Bwana
Ni wewe Bwana
Haleluyaa huuuu!
Ni wewe uliyenitoa mbali
Ni wewe uliyenishika mkono
Ni wewe uliyenivusha majaribu
Ni wewe uliyeniinua
Ni wewe Bwana wangu
Ni wewe Uliyefanya yote
Ni wewe Bwana wangu
Ni wewe Jemedari wangu
Haleluya!
***