Unikumbuke Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2021
Lyrics
Unikumbuke - Ambwene Mwasongwe
...
nimekuita waambie watu ushuhuda wangu
miaka tisa nimekaa jela
nilifungwa kwa kosa lakusingiziwa
namshukuru Mungu nimetoka..
Usiku ule nilikamatwa kama mchezo na mke wangu na Mtoto mdogo
nikadhani labda walikua wanatania, labda ilikua siku ya wajinga
Hakuna mtu alielewa ukweli wa maneno ya ushahidi wangu,
wala sikua na wakumueleza akanielewa
Mazingira ya kesi, ushahidi, sheria za kazi zilibana mpaka mke wangu kaniambia kama umefanya kiri kosa tujue moja
Unikumbuke ( Kumbuka haki yangu sikufanya ubaya) Nikumbuke (kumbuka sikufanya ubaya)
Nikumbuke (Namna walivyo nishtaki kwa hila na wivu)
Nikumbuke ( Bwana unikumbuke mimi eeh..kumbuka Bwana haki yangu)
Uwakumbuke (mke wangu alivyokufa nikiwa jela) Uwakumbuke (Kaungua kwa moto akiwasha mshumaa ndani ya nyumba) Uwakumbuke (mkumbuke mtoto mchanga asie na hatia) Uwakumbuke (kama ningekuepo angepona) Mkumbuke dada aliye baki alikufa kwa mshituko kwa ajili yangu
Nilidhani Mungu kalisahau file langu, nikadhani kwamba nitaaibika , sikuwa tena na tumaini lililopangwa, haki yangu ilikua tumaini pekee
waweza elewa shahidi wangu alikua Mungu labda na wale walio ua mwisho wa siku Mungu alinitetea wa walio fanya kosa kuonekana
Haki yangu ikastawi kama Mtende na mweli wa Lebanoni
walinichimba hawakuning'oa,sababu ya Mungu waliniinamisha hawakunivunja, Walinitikisa sikupukutika, walinichuma ili niishe eeh Bwana ulinitetea na haki yangu
Unikumbuke ( Kumbuka adui walivyonizunguka)
Unikumbuke ( Kumbuka ushahidi wa maneno yao)
unikumbuke ( Kumbuka walivyonichafua jina langu)
unikumbuke ( Kumbuka walivyoniona kuwa ni dhaifu ukalisafishe jina langu)
Uwakumbuke ( Wakumbuke ukarehemu makosa yao)
Uwakumbuke (Japo walifanya ubaya Mungu wasamehe)
Uwakumbuke ( Nilienda Jela nikiwa bado sikujui)
Uwakumbuke ( Nimetoka nimeokoka Nakujua, Nikumbuke Bwana Unikumbuke usinisahau)
Natangaza Fadhili zako
Nimekumbukwa, Nimefurahi