Alisema Lyrics
- Genre:Afrobeats
- Year of Release:2018
Lyrics
Alisema - Nay Wa Mitego
...
Alisema alisema
Alisema nyerere Alisema
vijana wote na tuamke na sasa tuanze mchakamchaka
Alisema Alisema
Alisema mwalimu Alisema
vijana wote na tuamke na sasa tuanze mchakamchaka
ni dhambi kukaa kimya
ni dhambi kutokemea
kwa maovu na ukatili unaotokea
najaribu kukaa kimya ila nafsi inanisuta
hata usiposema na bado yatakukuta
ni bora ukasema sasa mana wakati ni ukuta
vijana wamepewa madaraka wanatukana wazee
hivi mnadhani mtakuwa viongozi milele
mungu yupo acha tuone uko mbele
naona hofu imetanda watu wanaogopa kusema
maisha yamekuwa magumu nayo mnaogopa kusema
acheni uoga kuhisi mtakufa mapema
rest in peace Akwilina mungu akulaze pema
kesi ya kifo chako huku bado ni lawama
mama ananikumbusha watoto bado wanasoma
mwanangu kaa kimya usije kamatwa tena
sawa mama hii ya mwisho naapa siongei tena ila
Alisema Alisema
Alisema nyerere Alisema
vijana wote na tuamke na sasa tuanze mchakamchaka
Alisema Alisema
Alisema mwalimu Alisema
vijana wote na tuamke na sasa tuanze mchakamchaka
siyo Kitan tu ata walio maofisin
pesa imekuwa ngumu lawama zote kwa John
mwalimu lawama zao zote Kwa John
wakulima lawama zao zote kwa John
wafanyabiashara nao lawama zao zote kwa John
bodaboda, bajaji nao lawama zao zote kwa John
wamachinga, wàvuvi nao (zote kwa John)
yapo mazuri anayofanya hongera ziende kwa John
mi naona anajenga sasa kusema
zipo mbeleni
jua kuwa mpinzani sio kupinga kila kitu (no)
lengo ni moja tu kuijenga nchi yetu
hakuna mbunge wala raisi wakukuletea chakula
kukupa kazi kisa ulimpigia kura
ufanye kazi na ndo upate chakula
nawaskia wabongo eti mnaitaka vita
mnaitaka vita ivi mnaijua vita
iza karibia na Kongo mpaka Leo wanajuta
ila isiwe sababu ya kutufanya tukae kimya
kiongozi akizingua hatumwachi tunamchana
poleni waandishi wa habari kazi yenu imekuwa ngumu
izo ni changamoto tu msikimbie majukumu
mama ananikumbusha watoto bado wanasoma
mwanangu kaa kimya usije kamatwa tena
sawa mama hii mwisho naapa siongei tena ila
Alisema Alisema
Alisema nyerere Alisema
vijana wote na tuamke na sasa tuanze mchakamchaka
Alisema Alisema
Alisema mwalimu Alisema
vijana wote na tuamke na sasa tuanze mchakamchaka
mmmmh mmmh mm