Hesabu Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2021
Lyrics
Hesabu - Bando MC
...
Shy town boy yeah
Muungwana nishachutama niwe zuzu ama zoba maana alinisomesha mama kwa msaada wa nguvu ya vikoba uswazi kuwa winga kwenye dagi nyuki nitakaa mizinga yote ila sio mzinga wa konyagi
Nawapa vidonge wako hoi nina hasira kiasi cha kumpiga konde hadi konde boy
Ikiwa mbichi watachagua na wabongo wanaamini kwamba bongo hakuna mbishi kama Muhaa na siku hizi naona ukubwa bajeti na ukiamini kwamba mtoto ni mchanga basi mkubwa sementi
Ukitaka ujiseti hoi nakupa somo ukiona demu amepewa shavu ujue amegawa mdomo tupa shuka mwana Sinza kumekucha hata mwenye kipara ukifika kimalasuta mapenzi ya bongo ukiyapa chance yanakutesa wenye pesa hawana mapenzi wenye mapenzi hawana pesa
Nataka kunya…kunyanyua mike eeh bwana nataka kunya…kunyanyua mike x4
Na ukiniona sijanyoa ujue uchebe namtuzianga Shishi nampa tofali domo zege atajengea ndichi kutafuta ubikra kwa Amber Rutty ni kulazimisha kitambaa cha leso ukishonee suti
Kupenda moyo ndio maana moyo unaumia kutoa ni moyo na kujumlisha ni moyo pia moyo ungebaki single tu kusukuma harakati moyo wa mama ntilie ungesukuma chapati aah wanaelewa kina Dangote bar moja kwenye verse wanalewa ma-rapper wote wasojua kuchana na hawajui punch line wakichana punch zao zinakua punch laini huu mziki hauna haki unavyosukwa inachanganya wananyimwa haki aki na ukwa sishangae wanao win akili sufuri namshangaa demu wako anaenda mwezini bila nauli
Nataka kunya…kunyanyua mike eeh
Bwana nataka kunya…kunyanyua mike x4
Eeh Mungu ulenipa akili ya kutambaa Leo nasimama paka walionipa kiti wanakaa
Wanashangaaa, milele naomba niwe hivi kinacha wengi ngedere usishangae wakipenda ndizi nacho jifunza ni kubaki mwangalifu yani kiufupi bongo hakuna fundi mwaminifu ukijitahidi utanisoma ukiona kiziwi anaskia baridi ujue ndio ameanza kupona iko wazi madada mjini wanadanga ni kwli kwamba wenye vipara wengi wanawanga ulimbukeni tabu uchizi dili we boya uliyefuta namba ya demu wako na kichwani umeikariri
Mziki kuku naunyatia polepole na uchinjwe kwa dua ya kilokole ntawapa kipapatio wanangu am sorry ila masnitch ntawapa miguu wakatiane vidole
Nataka kunya…kunyanyua mike eeh
Bwana Nataka kunya…kunyanyua mike x4