Segerea ft. Kontawa & Xouh Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2023
Lyrics
Segerea ft. Kontawa & Xouh - Bando MC
...
mmmmh Mi nachekaga tu
J dramer on the beat
Segerea
Segerea
Segerea
Segerea
Segeraa
Segerea
Aaah undugu unapimwa nyakati ya shida sio kushare majina ya ukoo
Au kushare sare za msiba huku unakijiba cha roho
Ukitaka kujua rafiki wa kweli ni yupi yupi ni yupi ni urafiki ambao utazidi urafiki wa tako na chupi
Nipo jela sasa yapata mwaka na myezi kumi sijaona mjomba sijaona kaka ote wamenitupia kapuni
hali ni duni tuseme Labda suala la uchumi ndo washindwe kuniletea hata kipande cha sabuni
Maneno ya mama angu yananiumiza sana kila akija kunisalimia ananiliza sana ananiambia aoni thamani ya maisha yake mana me ndo jembe kwenye kila shamba lake
Inaniingia huruma kama mzazi mwanangu anapokosa huduma hata ya mavazi huduma hata ya shule ambayo itamjengea future kila msaada kazi bure wengi wanamjengea tuta
Daaah inanipotezea amani hata nilio wapa mwanga nao wamepptelea gizani
Ahsante kwakupata chance ya kuja kunitembelea karibu sege dance nyie mnapaita segerea
Segerea
Segerea
Segerea
Segerea
Segeraa
Segerea
Aah watakuambia jela ni jeshi watakuambia jela ni chuo pitia mafunzo yote ila bhana jela kituo mwanakwetu jela ni shile ambayp mtoto usimsomeshe kuingia ni bure ila kutoka ndo kasheshe
Ugali ndondo daily huku hawazongatii mapishi na wapo walio zoea wakitoka watarudi ndichi
Kuna mwana kamaliza kifungo haijakata wiki kakamatwa akiwa anauza bangi kituo cha police
Wapo wenye kesi za ufujaji,za mauaji,za utekaji,za ukabaji,za uporaji,uzurulaji na ujambazi wapo walio fungwa bila hatiaila siri ya mlango imefichwa nyuma ya pazia
Nimeona viini machp nimeona michakato hakuna yesu mwenye haki mbele ya utawala wa pilato nimeona mengi huku kuna mangavwaliingia malijali ila wametoka wakiwa wamesha left group
egerea
Segerea
Segerea
Segerea
Segeraa
Segerea
hebu kwanza niambia chakula cha jela unashiba
Najua jela hakuna amani hata ukiingia na frida jitahidi kuwa mvumilivu vumilia ma niga hata uwe na mbio vipi huwezi ukazimbia shida
Ona kesi sio yako na umeingia jela umeacha mama na watoto wanateseka kisa hela
Kiukweli sikufichi kuna watu wanakela mtu kakabwa na tonge alafu anasingizia masela
We sio wakwanza kufungwa usitie unyonge kirahisi maana hata yanga ashawahi kufungwa na police
Huku mtaani maji hayatoki na hivyo ndo tunavyo ishi so ukiskia mtu anaoga jua anaoga matusi
Jela tumeumbiwa watu usiumie kuwa kwenye hilo jumba me mwenyewe nipo mtaania lakin huko ninachumba
Bongo ukitembea na mwanafunzi unafungwa ila yesu alitembea na wanafunzi na hajafungwa
Segerea
Segerea
Segerea
Segerea
Segeraa
Segerea