Kiulaini ft.Makamua Lyrics
- Genre:Afrobeats
- Year of Release:2008
Lyrics
Kiulaini ft.Makamua - Mh Temba
...
Nafungua kurasa, ya binti kumnasa
Afike kwetu kiumeni (kiulaini)
Kumchanganya changanya, kumdanganya danganya
Afike kwetu kiumeni (kiulaini)
Nagundua ni rahisi kama kibogoyo tu kutafuna maini (kiulaini)
Usiogope naitwa Temba, sijawahi kukasirika
Na tena nahisi sina dhambi, ukinikataa umenipa dhambi
Ya nini uniogope wakati usoni sina hata tope?
Waenda wapi twende wote, tukapate hata chochote
Nipo tayari kwa lolote
Punguza hasira mamaa
Ungejua nilivyokupangia mwenyewe ungekuja kiulaini
Mtoto laini hata kuvunja biskuti hawezi
Anaishi Mbezi, mi namzimia kishenzi
Nikamwambia una wasiwasi gani? Mi nasoma chuo marekani
Baba yangu na mama yangu wote wapo serikalini
Baba waziri wa madini, mama mbunge kwetu kijijini
Tulia na mimi Temba mtoto wa mjini
Utajinyima zali wakati unaonekana kwenu njaa kali
Akaniangalia kwa dharau, akatema mate chini
Huyu queen, nikajua leo nishapigwa chini
Nikamwambia naomba tukapate lunch
Akasema, "mi staki"
Nikamwambia naomba namba ya simu
Akasema, "mi staki"
Akawa anaondoka nikamwambia nikupe lift
Basi akakubali mtoto mzuri kimwali
Tukazama ndani ya gari shori mwenyewe kapagawa
Full ma-air fresh, upupwe kideo ndani
Yaani live channel 5, The Comedy walee
Pembeni kuna kifriji nikavuta nikamtolea kyoda
Anywe asikie uroda
Ajamaliza kunywa, kama masihara
Nkambinyia kiti akalala
Tumefika mbele nikamuuliza, hujafika unapoenda?
Akadai anaenda popote mi ninakokwenda
Nikasema ndo maana yake, kwisha jeuri yake
Ah, jamani
Nafungua kurasa, ya binti kumnasa
Afike kwetu kiumeni (kiulaini)
Kumchanganya changanya, kumdanganya danganya
Afike kwetu kiumeni (kiulaini)
Nagundua ni rahisi kama kibogoyo tu kutafuna maini (kiulaini)
Wale kiulaini, wale kiulaini chini chini
Brake air apartment parking kwa Mwakamere
Mtoto namwambia agiza ndo kwanza anacheka cheka
Kaulizia bei wine, kaambiwa laki anasema hataki
Nikamwambia agiza wewe, tena bila kuuliza
Mtoto kaona kama miujiza kaenda Ulaya bila visa
Nia yangu nimchanganye, ndio nikambane
Tukahama pale walee, tukaenda bar moja Kongowe
Bar ina vituko, ndani wahudumu nyani!
Bia buku 5, soda elfu mbili mia tano
Kwenye mabano kiingilio buku kumi na tano
Tumeingia tu anadai anasikia usingizi
Nikamwambia ngoja ngoja, hapa moja moja
Nikamwambia utalala wapi, akadai popote
Nikamwambia, "kwenye gari?" (an ah)
"Hapa hapa?" (an ah)
"Wapi sasa?" (Chumbani honey)
Huku sauti anaitolea puani, eti twende chumbani honey!
Nikashangaa mara hii nishakuwa honey, ama ananiletea utani?
Yaani kiulaini laini hivi leo najibebea mzigo!
Basi kukawa hakuna budi, sikataka mwenyewe
Nikimuacha ataona namuogopa, tena ataniona rofa
Basi nikawa sina jinsi kwa huyu miss
Kwa kuwa si kataka mwenyewe
Ah, bora nikamshugulikie ili vizuri kwa wenzie akawahadithie
Awaambie mi ndie tabibu nilietibu taratibu
Basi nikamshughulikia, wala hakulia
Alifurahia akaniuliza lini tutarudia
Nikamwambia, "kesho baby, kesho!
Tuipige again mechi"
Nafungua kurasa, ya binti kumnasa
Afike kwetu kiumeni (kiulaini)
Kumchanganya changanya, kumdanganya danganya
Afike kwetu kiumeni (kiulaini)
Nagundua ni rahisi kama kibogoyo tu kutafuna maini (kiulaini)