Amekoma ft. Q Chief Lyrics
- Genre:Afrobeats
- Year of Release:2007
Lyrics
Amekoma ft. Q Chief - Mh Temba
...
chorous
Amekoma amekoma amekoma
Amekoma amekooma amekoma
Alidhani poa poa kumbe sio poa aaah side mnyamwezi
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi
Verse 1
Anaitwa side said mnyamwezi mtoto wa mbezi
Mtu wakulipuka pamba ile kishenzi
Anamiliki prado colora pamoja na benzi
Ni kijana mcheshi mtanashati ushauri huwa hataki
Matumizi yake kwa siku yanazid laki
mimi namsimulia story yake sababu nimekua naye huyu nimesoma naye huyu hata sasa nishagombana nae
Wazazi walimshauri huyu akawana kiburi
Hakuwa na malengo wala dira kama taila
Ni mwongo mtoa fix wa kuaribu mabinti
Hana mapenzi ya kweli analaghai wakina dada
Mwishowe aliwatelekeza bila kutoa msaada
Alikuwa mpenda sifa demu wake wa kwanza alikuwa Latifa
Penzi halikudumu sana miezi kadhaa wakaachana
Hii ilikuwa furaha kwake kashamaliza haja zake yule akaenda zake
Akaja akang'oa mwingine alikuwa ni demu wa rafiki yake
Yeye hatambui hilo anahamishia tu kwake
Na juzi kafumwa guest na mtoto wa dada yake
Tabia yake na mambo yake wengi hawakuipenda
Masela mtaani washapanga dili wampige mawe
Wazee wamekaa vikao wanatamani wamuue
Huyu jamaa wanamwita Kiwembe hywa abakizi demu
Mtaani alimpaka razia tukajua anamchumbia
Kila siku anaye kwenye gari wanakula raha za dunia
Alimgharamia mpaka tukajua anaona
Kumbe maisha ya yule binti anaenda kuyatia doa
Razia atake nini asipewe chochote kisichelewe utasikia nataka gari
Tulia ntakupa nataka simu usihofu ntakupa
Hii tabia sijui amerithi au unelogezewa
Anayoyafanya jamani nahisi ametumwa na shetani
kashagombana na rafiki zake kisa wanawake
Side huyo
chorous
Amekoma amekoma amekoma
Amekoma amekoma amekoma
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi
verse 2
Side huyo side huyo mnyamwezi huyu hapa tena
Akishamaliza anatema aliendelea na tabia yake ili afurahishe moyo wake
Alishapata kesi ya kumtorosha mwanafunzi
Na hivi juzi juzi badala ya kung'oa demu kang'oa shoga
Akaenda kula kiboga bila woga
Kwa tabia yake ya kishenzi akashindwa kuishi mbezi
Akaja akahamia Chang'ombe akapata demu Shombe Shombe anakunywa pombe
Alimlea vizuri akamhonga mpaka gari kwao akatoa mahali
Ni starehe juu ya starehe wanakula raha mazee
Kwa kuwa alikuwa nao wengi hakujua amchukue amuoe yupi
Alhamisi ladies is free kama kawaida billcanas
Akaenda akang'oa mlupo alikuwa na rafiki zake akawatelekeza wenzake
Eti kisa demu ndio unawatelekeza masela
Aliondoka na yule demu akaenda kujipunzisha
Kumbe demu si demu demu mwenyewe anatisha popote utakapo mfikisha lazima atalianzisha
Vimbwanga vilipomkuta ilibidi side adate
Wamefika guest ndani picha linaanza
Demu nini... anataka kumvua kimini
Demu kaanguka chini anataka kumsogelea demu kapotea
Anataka kumkumbatia demu kageuka kawa ngamia
Side anaanza kulia anatafuta njia ya kukimbilia
Binti anaanza kubadilika sura za ajabu ajabu
Mara ratifa mara razia mara stella eh eh mara akageuka Rashidi
Ikabidi side atoke nduki guest uchi
Huku anapiga kelele kama mwizi au chizi
Walinzi wamemkosakosa walijua mwizi yuko uchi wa mnyama watu angali wanamtazama
Anaita mamamama kimefika kiama ikabidi waungwana wamsitiri kwa kumpa nguo
Anaapa amekoma Chang'ombe nzima anaona noma
Wiki nzima hii hajatoka nje anaona aibu kwa yaliyo msibu
Side huyo side huyo mnyamwezi
Yeah yeah
Chorous
Amekoma amekoma amekoma
Amekoma amekoma amekoma
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi
Q-chief
Anauza sura masaki anaishi geto Magomeni
Choo cha kulenga ugali tembele nyumba ya makuti side mnyamwezi
Wanaume walimwambia lakini wapi mchizi hakutaka kusikia kila tulichomwambia lakini wapi mchizi hataki kusikia
Jibu lake aaah wapi kwa machizi aaah wapi kwa masela aaah wapi
Chorous
Amekoma amekoma amekoma
Amekoma amekoma amekoma
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi
Alidhani poa poa kumbe so poa aaah side mnyamwezi