Almasi (feat. Tk Nendeze) Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2021
This song is not currently available in your region.
Lyrics
Almasi (feat. Tk Nendeze) - Dizasta Vina
...
Nilikutana mtaan na mzee mmoja
Tukaketi chini akanipa soga
Mimi sitamsahau
Alisema wangapi walikuwepo namba Moja
Sasa wamerudi chini ni Vioja
Watu wamewasahau
Utavamia kwenye Tamasha la Muziki
Usoni bashasha huku rohoni umekumbata Dhiki
Sanaa imesanda na Sasa tena hauna Kiki
Utaigiza Furaha Kwa kunywa bia za mashabiki
Zitaongea nguo ulizoazima Kwa msela hazitatosha kuficha ukweli kwamba hauna hela
Hautakumbukwa kama mwanzo kipindi unatisha Paparazi hawatakujua Hautapigwa hata Picha
Hakuna ataekuangalia Usoni
Tamasha utaingia kwa iuzidandia Kuponi
Mchumba uliemwaga atang'ang'aniwa kiunoni Utatabasamu huku hasira umeifungia moyoni
Utapotaka kujichanganya utahisi haya
Lips denda zitachakaa kusiz Kaya
Wataskika wadadisi wakiongea Kwa kudisi kamera zote zitamfata msanii uliomu-Inspire
Hayatakuwepo Majumba magari na Mapochi Nene Milo ya Hoteli za kifahari na marosti kede
Zitasahaulika idadi ya tuzo ulizohodhi kwenye majukwaa huku magazeti yakikuposti mbele
Hautatembeza tena Rungu ka Kipepe hautavutia wachuchu mana nyota haina nguvu
Hautafatwa tena na Mashushushu Kwa maseke Utakumbuka ulivozungukwa na grupu la Vicheche
Mchuzi utakauka utapiga hodi ukame hautawekwa kwenye Mabodi ka Van Damme
Hautashawishi magari road yapangane na utakuwa pekeako bila ya Ma-Boardguard nane
Kipindi ambacho Taswira yako ipo gado ndo kipindi Cha kulikata shauri lako kutambua nafasi na thamani ya sauti yako
Kutambua dhamana mwanzoni kabla ya mauti yako
Dhamana yako ni zaidi ya kula na kupiga pamba Kali kununua Chupa na bupa na ukizilaza chali
Jina kubwa likikufumba ushindwe tafakari utakufa Maskini ukizubaa kuzichanga mali
Usije sahau maisha yako Halisi yanayolingana na kipato chako thabiti
Usije kufa kipindi ambacho michango haikidhi haitoshi hata kujenga nyumba ya Mamaako Kibiti
Uko wakati wa kumiliki idhini ya uongo wako
Wenzako wamedondoka
Je.? Utajifunza
Unasifika mjini Kwa wingi wa Longo zako Ukifa Tutasimulia nini watoto wako
Tutasimulia idadi ya totoz ulizonusa.?
Au Gambe idadi ya kopo ulizoruka.?
Idadi ya mahusiano na mioyo uliyoivunja au idadi ya wasichana wadogo Ulowavuruga.?
Najua mwisho mwanang hamna njia Utatokewa na Kila Hadithi unayoiskia (unayoiskia)
Sicho kitu ninachohofia Hofu yangu kama umeiandaa saikolojia
Ukija wakati pazia Halifunguki wadananda waliokudandia hawakukumbuki
Najua itafanya akili ichoke Utapagawa Tafadhari usijegeukia pombe na madawa
Kipandacho hushuka ulishawaza (ulishawaza)
Si miujiza ni asili inayoshangaza (inayoshangaza)
Wasahaulifu wa ulimwengu walitangazwa watatajwa mashujaa na Jina lako halitatajwa
Wanafki walafi na mabishoo zako
Wangapi watakuwepo kiu ikidaka Koo lako
Muda wa kuwasoma wote walioko kando yako
Mana hata pesa haitatibu jeraha la Roho yako
Maagano ya hii Siri yatakuwinda
Vyote walivotabiri vitafika
Maisha ya ndoto yataisha utairudia kawaida utagundua kuwa haukuwa Malaika
Kiasi utaijua dini Utaijua harufu ya Sakafu kwa mana utakuwa chini
Hata maana ya maisha itapotea Sumu, Kisu na vitanzi vitasogea
Sikutushi ila utakufa pekeako Jeneza lako halitabebwa na hao Vicheche wako
Sishangai wenge lako ng'ombe nashangaa unapoyumba kwa kuzidiwa na ukubwa wa pembe lako
Ni Heri kuwa Mwewe
Mana muoga anajali kua Uelelewe
Kundi la watoto nyumbani wanakupenda na wanaota siku Moja waje kuwa kama wewe
.....
..........
(Lyrics by AT Man Don )