Loading...

Download
  • Genre:Hip Hop & Rap
  • Year of Release:2021

Lyrics

Kanisa rylics

Yoh!

Salamu kanisa wako mpendwa katika bwana

Katika wana waliotaka kufeli nami nazama

Tangu jana uwepo wako haupingiki

Kisa una nguvu ya kuwavuta wasiosadiki


Sikuhitaji mambo ya kugawana madhehebu

Waumini dhaifu wanahama hama kama wehu

Ikiwa tangu kale wazazi wangu walichanganywa

Basi hakika sitahukumiwa kwa kudanganywa

(Kanisa)


Sidhani ka' upo sawa kunibeza

Maana hata wewe unapitisha dawa za kulevya

Tukianza ku-confess yaliyo nyuma ya pazia

We utachomwa moto alafu mi nitaachwa nakuapia


Sitaki kuamini kuwa sadaka au kusifu kwa fasihi

Ndio vitanipeleka kwa masihi

Kitachonionyesha mbingu ni bidii

Ya kutenda mema so sitaki kujua dini ipi ni sahihi, ah!


Kanisa unatudanganya kirahisi

Nyumba ya mungu ni mioyo yetu nahakiki

Kwakuwa saa hizi

Jua kali njaa hizi zinafanya ukubali kugeuka taasisi


Usinishushe hadhi nikizini

Ikiwa unafuga wachungaji wenye dhambi kama mimi

Kanisa nakupa pole

Nje msafi ndani mchafu naomba tusinyoosheane vidole


Kanisa unaniasa

Niache kutamani vyeo na wewe unajihusisha na siasa

Kama mji wa sodoma ulizikwa na anasa

Mwisho wako upo kama hautabadilika sasa


Haufanani na meli ya nuhu

Unaniomba mchango na kodi nimefeli kumudu

Kanisa unanitapeli kizungu

Unanizungusha haunionyeshi kanisa la kweli la mungu


Eti manabii wana vyeti

Kanisa lina account ya mitandao ya kijamii mpaka benki

Wahubiri wanavutana kinguvu

Kanisa unajitangaza kutafuta umaarufu?


Unapishana na muda hakika

Unachojua pekee we ni kufa kuzika

Unanishauri nije kwako ndoa ikiyumba kanisa

Kichekesho kwamba wewe ndio umeyumba kabisa ah!!


Kanisa nilikuja uniongoze

Nimpende mungu wewe unaifunza nimwogope

Jua kali lilinifunza kukaba nikakupa maisha

Na cha ajabu haujanifunza chochote


Nasikia una pande mbili za sarafu

Upande mzuri na upande unaoingia dili mpaka na wafu

Na unanifundisha baya haliwi na thawabu

Nilikuwa mjinga na sasa nayabashiri majawabu


Tunahitaji mafunzo halisia

Wakati mbinu zako zimejaa mafumbo na sheria

Kanisa tunaishi na wanafki kudadeki

Unajifanya rafiki sababu ya ulafi wa chenchi


Ikiwa huruma ya jah haina kipimo

Basi kati ya wanaoomba msamaha nami nimo

Dhambi zako sawa? Tumezidiana kimo

Mungu aliye hai akuepushie shimo, kanisa huh!


Umeshindwa kukidhi

Utu unakutoka sababu umeshikwa na dhiki

Unasahau lengo unasahau umesimamishwa na sisi

Pesa inakuyumbisha nawe unayumbisha misingi


Kijiwe chako hakikuniingia akilini

Nikafata vijiwe vya pombe vikanitia umasikini

Kisa kila aliyenionyesha nia nilimuamini

Leo siwaoni wote wameingia mitini


Haupo hata kwenye hadhi ya utatu

Mungu baba, mwana, roho kisa kazi za uchafu

Kanisa hauchezi Pasi ni rafu

Unaremba altale kuliko hata nafsi za watu


Kwa sasa ninahisi una bifu

Na taasisi binafsi kwa sababu haukuwa mwangalifu

Kama ndani yako wanaoishi wadanganyifu

Na wanasali hautazalisha watakatifu


Kuwa mkweli ni wapi ulipoishindwa nielewe

Hiyo siri yako hauwezi ukaificha milele

Kama nitachomwa moto wa kukushika ni wewe

Nishakusafisha kuliko kujisafisha mwenyewe aah!!

Similar Songs

+

      -   or   -

      -   or   -

      NG +234

          Please Select A Playlist

          Add New Playlist

          Share on

          Embed: Love & Light EP

          Custom Size :

          • Default
          • Desktop(300*600)
          • Mobile(300*250)

          Type :

          • HTML/HTML5 (WordPress Supported)
          Get Boomplay Premium
          for
          Payment Method
          Pay With
            Review and pay
            Order Date
            Payment Method
            Due Today
            Flutterwave
              Subscription Successful

              Congratulations! You have successfully activated Boomplay 1 Month Premium.

              Now you have access to all the features of Boomplay App.
              Payment Failed

              Please check your balance and then try again.

              You'll lose your subscription if we don't have a working payment method for your account, so please check your payment details.
              Need help? Contact Boomplay Subscription Support.
              Payment Processing...
              10 s

              Payment is being processed by . Please wait while the order is being comfirmed.

              Payment Processing
              Your order is processing, and it may take up to a few days for the service provider to handle your payment. Please kindly stay tuned and check your order status in ‘User Center’.
              About Order Status