Nipeni maua yangu ft. Abiud Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2023
Lyrics
Nipeni maua yangu ft. Abiud - Roma Mkatoliki
...
Wamemchokoza Bea!
Tumekumisi Roma
Rudi nyumbani Roma
Uwatetee wanyonge ndugu zako
Uwakumbushe viongozi
Sasa sijui nianzie wapi kifuani nimebeba mengi
Na sitotenda haki nisiposema hiki sipendi
Hiki napenda kile sitaki mambo ya kishenzi
Tanzania haijaezekwa bati na wamekula pesa ya ujenzi
Yaani nchi wanaifanya mti mjenzi anauona mbao
Ndege ataona makazi mkulima ataona mazao
Mganga atauona dawa na mpishi atauona kuni
Ataemiliki mwenye power sisi atatusagia kunguni
Na ukisema hawatufai wanakuumiza uwe mpole
Yaani wanaangua papai kwa kutumia gobole
Wanatumia nguvu kubwa kwenye mambo madogo
Jeshi gani mpaka leo mmeshindwa kumjua kigogo
Tukiongelea kutekwa eti tunarudia ajenda
Hamjibu mnakwepa mbona mama anarudia kilemba
Nchi gani raia akihoji mnasema anakosoa
Na akikosoa anatukana serikali hii sio poa
Haya basi tuseme mko sawa na mna nia nzuri na sisi
Mbona vyuma vimekaza halafu mama anaificha grease
Mara mkapandisha tozo kampeni mkono hatuwaungi
Si tulihoji mkajibu kwa dharau tuhamie Burundi
Tatizo mkishaapishwa tu mnawaza uchaguzi ujao
Hamuwazi njia mbadala ya kumlinda mkulima na mazao
Sasa Iringa si tuna msitu halafu tuspick twaagiza China
Manaake hapo kwanza ncheke yaani Bongo kikubwa uzima tu
Sa mnatuambia tujiajiri mbona nyinyi hamkujiajiri Okay nikupe boda yangu kisha we unipe uwaziri
Nikukabidhi vyeti vyangu hangaika navyo mwezi mmoja
Niko pale nakungoja uje tuongee lugha moja
Mi sio CCM sio CHADEMA hili niliweke wazi
Ila ukiweka CCM na Andazi nitachagua Andazi
Simuamini mtawala na mpinzani simsadiki
Maana wanaendelea kukatika huku DJ kauzima mziki
Na inaniuma kuona kijana msomi wa degree tatu
Nashindwa kumpa ajira sasa anauza nyanya karatu
Sasa sijui mtaniua nikimshikia mama shilingi
Maana hata inyeshe mvua mnasema anaupiga mwingi
Na ninamkubali na nitamng’ata sikio kama hajui
Wanaomkosoa ndo wanampenda wanaomsifia ndo maadui
Ili wapate teuzi ndo wanamlamba miguu
Wakimpamba hawamsaidii Amiri Jeshi Mkuu
TUNAKUPENDA ROMA
TUNAKUMISS ROMA
RUDI NYUMBANI ROMA
UTUSEMEE
TUNAKUPENDA BABA
TUNAKUMISS MWANA
TUNAKUKUMBUKA SANA
Hivi hamjasikia tetesi kuwa remote iko msoga
Si huku mageng imedoda magogoni imenona
Watu tatu ndani ya track moja wamekalia kigoda
Ngolo Kante anampa Mbappe cross anafunga Pogba
Hii nchi ina wenye nchi walanchi na wananchi
Na kuendelea kuwachagua ni kwenda na mchanga mbichi
Tuwajaribu na wapinzani watawala si wameshapata
Ugoro umewaingia puani sasa ona wanapiga chafya
Wanatumia dollar kubaki kuongoza dollar
Watawafunga watapora wataua watahonga vijora
Karatasi tunaibiwa za kura kwenye sanduku
Kwa hiyo mnatuonyesha ziwa huku mmeziziba chuchu
Okay kura ziko 300 na kuna watu mia kwa jimbo
Na kituoni hakukua na watu halafu wameshinda kwa kishindo
Sa kama Askofu mfufua watu ameiba kura za mpinzani
Je atashindwa kuiba sadaka za waumini kanisani?
Hii ni gani mchungaji akitaka gari twamchangia
Muumini akitaka gari anaombewa tunamsalia
Sa mchungaji tusimpe pesa tumuombee na yeye pia
Tukae pale tusubiri miujiza ya wagalatia
Wabunge wengi mlishinda kwa hisani ya mwendazake
Mkipatacho muende Chato mkumbuke hata ndugu zake
Jimbo hili haliendelei cause mmemchagua mpinzani
Haya sasa mmeshinda kote fauluni huo mtihani
Turuhusu siasa za amani turudi zile enzi zetu
Uchaguzi sio siku moja ni mchakato wa muda mrefu
Mikutano ya nje na ndani ndo tunaimarisha chama
Daily mtulishe majani halafu sikukuu mtupe shawarma
Keki ya taifa ni kubwa tuache siasa za risasi
Mnawaonea wakishika dola watalipa kisasi
Tulipotoka ni mbali siasa za mwendazake
Msirudi msilale chali huku mnatutemea mate
Na BASATA msikie hili msije fungia huu wimbo
Kichwa kisicho na akili ni mzigo kwa shingo
Sawa tulinde maadili ila tusiue wabunifu
Mtupende tunaokosoa kama mpendavyo wanaosifu
Wengine wamekuwa viongozi na mliwaona tu marapa
Hiphop ni mkombozi na sauti isiyo na mipaka
Ushauliza kwanini bega lipo karibu na kwapa
Usiondoke baki hapa usikie verse inayofuata
(REPEAT CHORUS)