Acha Nikae Kimya Lyrics
- Genre:Afrobeats
- Year of Release:2017
This song is not currently available in your region.
Lyrics
Acha Nikae Kimya - Diamond Platnumz
...
Mmmhh... mhhh
Mama ananiambia Nasib mimi ni mtu mzima na we ndo nakutegemea
Yanayotokea Jaribu kupiga kimya usidiriki hata kuongea
Mara Nasikia vya Aibu Konda Gwajima eti ugomvi umekolea
Kuchunguza karibu ni binti mmoja kwa mitandao anachochea
Najariibu Kunyamaza, ila moyo utaki
Unaniambia eti simba japo nguruma uisemee haki
Oooh Najaribu kunyamaza hata Laizer hataki ooh
Anasema walau nena kidogo
Na mashabiki Dangote, wananiambia mbona husemi chochote ah si uko nao siku zote
ama ulezi unafanya uogope ah na media pande zote wanalalama Kiongozi Atoke
Nchi inaingia matope, niende wapi na mi mtoto wa wote
Acha nikae kimya(nisiongee)
(Kimya)Ooh ninyamaze mimi
Nikae kimya, Nisiseme(kimya)
Mama kanambia(wacha nikae kimya)
Oooh nifunge mdomo(kimya)
Mie bado mdogo sana, nisiseme(kimya)
Mmmh Ni mengi majaribu najitahidi epuka yasijenicost
Japo mengine Swadakta Mengine hayana Maana
Rafiki kipenzi wakaribu ata nyimbo yake sikueza ipost ila alivokamatwa iliniumiza sana
Mitandao kila kona
Uongo na Ukweli unashonwa, Kila nyumba inanong'ona
Aaah Ooh Tanzania
Mara kimbembe Dodoma Bunge wapinzani wamegoma
Juzi akapotea na Roma
Ooooooh Tanzania ooooh
Najariiibu kunyamaza, Makame hataki oooh eh
Ananiambia walau nena kidogo
Nyumbani Nafungua Geti niende kwa mangi nunua spaghetti eeh napewa za chini ya kapeti
Kuna Redio imevamiwa eti
Eeh Napita kwenye Magazeti Nakuta Rundo la watu Wameketi eeh badala ya kutafuta set wanabishana tu mambo ya vyeti
Wacha nikae kimya(oh nisiongee)
(Kimya)Ninyamaze Kabisa(nikae kimya)
Ulimi Koma(Kimya)Usijekuniponza(wacha nikae kimya)
Nifunge bakuli langu nikojoe nikalale
Me bado mudogo sana(Kimya)
Mama kanambia
Ooooh Najiulizaaa(ooooaaah)
Najiuliiza(oooah)
Tunakwenda wapi(waaapi)
Kila siku maneno
Ah tuacheni Jamani
Me na we ni taifa moja
Kambarage baba mmoja
Sa tofauti za nini tushikamane
Tukaijenge Tanzania