Ni Mwaminifu Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2023
Lyrics
Ni mwaminifu mungu wetu ni mwenye nguvu,
Hayumo kwa wafu ameshinda kifo,
Ushindi mkubwa kwa mwana wa adamu,
Kwa kifo chake tumepata ukombozi,
Anyenyekae kutazama mbinguni,
Atapata uzima milele,
Atakuinua mnyonge kutoka mavumbini,
Akuketishe na wakuu
Twenende kwa njia zake,
Tusimtafute kwa wafu kwani yesu amefufuka,
Mtafute aliye hai,
Utoke miongoni mwa wafu akusafi,
Hatuna budi kutangaza,
Wema wake ulimwenguni,
Mataifa wasikie neno hili la ukombozi
Linda imani usimame kidete mpendwa,
Kwani wokovu umehakikishwa,
Toka kwa wafu uje kwa yesu kristo,
Aongoze mienendo na mawazo yako,
Uwe chumvi na mwanga kwa walimwengu,
Kama vinondo wavute kwa yesu,
Arudipo mwenye nuru uwe kwenye kundi lile,
Kwenye meza ile ya kifalme
Twenende kwa njia zake,
Tusimtafute kwa wafu kwani yesu amefufuka,
Mtafute aliye hai,
Utoke miongoni mwa wafu akusafi,
Hatuna budi kutangaza,
Wema wake ulimwenguni,
Mataifa wasikie neno hili la ukombozi