Dunga Mawe Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2023
Lyrics
Dunga Mawe - Kontawa
...
DUNGA MAWE
Anaitwa dunga mawe,
Mwanangu wa utoto,
Katika kitu nakumbuka,
Alipitia changamoto,
Mwanangu dunga mawe,
Alikuwaga kibokoo,
Na sura yake ilitumika,
Kutishia watoto,
Eeee
Oya huyo mwanangu alikuwa msela,
ALishawahi kufungwa akatoroka jela,
Maisha yake visanga yani mpelampela,
Asa ngoja niwape movie hilo lilikuwa twela
Eeee
Kuna kipindi dunga mawe si alipata mwali
Tukaenda hadi ukweni si kutoa mahali,
Baada ya vitu kukamilika tulivyopewa
mwali,
Akamvizia baba mkwe akamwibia mahali,
Alianza kuvata bangi na miaka saba,
Ulivyo wa nane akaanza kukaba,
Sababu ya hali ngumu kakosa msaada,
Eee
Hakuwahi kuwa na mama wala huyo babaa,
Ndugu wa karibu hawakumpa faraja,
Mali alizoachiwa na wazazi waakee kadhurumiwaa
Aaaah aah
Anaitwa dunga mawe
Aaah aaah
Mwanangu dunga mawe
Aaah aah
Anaitwa dunga maawe
Aaah aaah
Mwanangu dunga mawe
Ukimletea unyonge lazima aruke nawe,
Bora ukabwe na tonge ila sio dunga mawe,
Utafanya kitu gani hili umfanye apagawe,
Kashaoga matusi mpaka akaamua anawe
Ile siku dunga mawe akiamka vizuri,
Tena ukamkuta kwenye mood,
Anaweza agiza bia mbili,
Afu akakupa mia mbili,
Kisha akasema kwamba chenji inarudii
Demu wake dunga mawe alikuwa na mimba,
Yapata kama miez tisa,
Kwa kuwa pesa ya uzazi ilimshinda,
Ikabidi awe anapinisha,
Akamwambia kwamba mpenzi wake kuwa amepata safari,
Anaenda kupambana hili mambo yawe shwari,
Na atakaporudi watakwenda hospitali,
Aaaahh
Eeee
Kumbe alipanga kwenda kuiba huko sehemu za mbali,
Ndipo akakamatwa na watu wenye asira kali,
Wakamshushia kipigo,
Kipigo juu ya kipigo,
Namwisho wakamchoma na mipira ya magari
Aaaaa aaaah
Anaitwa dunga mawe
Aaaaa aaaah
Mwanangu dunga mawe
Aaaa aaaah
Anaitwa dunga maawe
Aaaa aaah
Mwanangu dunga mawe
Alianza kuvata bangi na miaka saba,
Ulivyo wa nane akaanza kukaba,
Sababu ya hali ngumu kakosa msaada,
Eeeee
Hakuwahi kuwa na mama wala huyo babaa,
Ndugu wa karibu hawakumpa faraja,
Mali alizoachiwa na wazazi waakee kadhurumiwaa.
Aaaaa aaaah
Anaitwa dunga mawe
Aaaaa aaaah
Mwanangu dunga mawe
Aaaa aaaah
Anaitwa dunga maawe
Aaaa aaah
Mwanangu dunga mawe