Nimeridhia Lyrics
- Genre:Bongo Flava
- Year of Release:2022
Lyrics
Nimeridhia - Maua Sama
...
Kwa goti aliingia
Nakutaka nimsamehe
Kumbe ananichora
Mapenzi yalinijia
Kwenye moyo shurba tele
Ya-radhi akanijia
Kidudu mtu shetani akayavuruga
Akaingia mashakani tukashindwana
Kidudu mtu shetani akayavuruga
Akaingia mashakani tukakwazana
Nimeamini kwenye moyo huwezi penda mara mbili
Penzi ukalitia kasoro maskini mimi
Moyo wangu sio godoro, uwe juu me niwe chini
Si kisoda kwa kokoro, nimeshindwa mimi yeah
Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi
Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi
Kweli sio siri, ilizingwa mapema
Tamu yako ya asili, ila ndani yachoma
Kheri kuwa dhahiri, maumivu kusema
Mlaghai kwa hili, nafsi yangu imenitenda
Nashukuru kwa kidogo, ulichonipa nimepokea
Nitabaki kwa mikogo, huyo mwingine kumngojea
Nimeamini kwenye moyo huwezi penda mara mbili
Penzi ukalitia kasoro maskini mimi
Moyo wangu sio godoro, uwe juu me niwe chini
Si kisoda kwa kokoro, nimeshindwa mimi yeah
Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi
Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi