DAIMA (LIVE) Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2023
Lyrics
Eeh Jehovah Jireh Mungu wangu uketiye kitini cha enzi
Mbele zako mi ninasujudu Wee ulo Mfalme wa wafalme
Eeh Baba yangu unapendeza Eeh Mungu wangu waheshimika
Uweponi mwako nasimama moyo wangu upate furaha
Daima nitakuinua daima nitakuinamia
Daima mi nitakusujudu eeh daima mi nitakuimbia
Daima nitakuinua daima nitakuinamia
Daima mi nitakusujudu eeh daima mi nitakuimbia
Eeh Muumba vyote mweza yote, Unenayo yote hutimia
Neno lako sawa nawe Baba hata wafalme walitambua
Maji baharini yasikia amri yako wee unaponena
Hata na dhoruba hutulia isikiapo sauti yako
Daima nitakuinua daima nitakuinamia
Daima mi nitakusujudu eeh daima mi nitakuimbia
Daima nitakuinua daima nitakuinamia
Daima mi nitakusujudu eeh daima mi nitakuimbia
Umetukuka wee toka jadi mbingu na dunia zafahamu
Masherafi nao makerubi waimba sifa'zo juu mbinguni
Duniani ndege wakusifu samaki majini wasujudu
Milima imesimama wima yangoja ukague gwaride
Daima nitakuinua daima nitakuinamia
Daima mi nitakusujudu eeh daima mi nitakuimbia
Daima nitakuinua daima nitakuinamia
Daima mi nitakusujudu eeh daima mi nitakuimbia
Daima dawama nakuinua Baba mi nitakuimbia
Mwamba wangu nakusujudu uishie mi nitakuimbia
Sauti yangu maishani mwangu nikuimbie mi nitakuimbia
Nikuabudu, nikuinue Mungu wangu mi nitakuimbia
Daima dawama nakuinua Baba mi nitakuimbia
Mwamba wangu nakusujudu uishie mi nitakuimbia
Sauti yangu maishani mwangu nikuimbie mi nitakuimbia
Nikuabudu, nikuimbie Mungu wangu mi nitakuimbia