Bwana Mungu Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2022
Lyrics
Bwana Mungu - Beatrice Mwaipaja
...
Bwana Mungu, nashangaa kabisa
Nikitazama kama vilivyo
Nyota, ngurumo, vitu vingi vyote
viumbwavyo kwa uwezo wako.
Bwana Mungu, nashangaa kabisa
Nikitazama kama vilivyo
Nyota, ngurumo, vitu vingi vyote
viumbwavyo kwa uwezo wako.
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.
(instrumental)
Nikitembea pote duniani,
Ndege huimba, nawasikia,
Milima hupendeza macho sana,
Upepo nao nafurahia
Nikitembea pote duniani,
Ndege huimba, nawasikia,
Milima hupendeza macho sana,
Upepo nao nafurahia
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.
(instrumental)
Nikikumbuka kama Wewe Mungu
Ulivyompeleka Mwanao,
Afe azichukue dhambi zetu,
Kuyatambua ni vigumu mno.
Nikikumbuka kama Wewe Mungu
Ulivyompeleka Mwanao,
Afe azichukue dhambi zetu,
Kuyatambua ni vigumu mno.
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.
(instrumental)
Yesu Mwokozi utakaporudi
Kunichukua kwenda Mbinguni,
Nitashukuru na kwimba milele,
Wote wajue jinsi ulivyo
Yesu Mwokozi utakaporudi
Kunichukua kwenda Mbinguni,
Nitashukuru na kwimba milele,
Wote wajue jinsi ulivyo
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.