Loading...

Download
  • Genre:World Music/Folklore
  • Year of Release:2022

Lyrics

Au ft. Nurwell - Nikki Mbishi

...

Yeah.. aah (ooooh)

I’m curious I wanna know (oooh mama)

Au labda hunipendi, ndo sababu unanitema

Hupendi ninavyoatend, alfajiri na mapema

Unaniacha stendi, njia panda niko dilema

Kutwa spendi weekend, kwako haijakaa njema

Au kisa silipuki, daily mitumba midosho

Ukiniona huzuzuki, sana sana unaona michosho

Bling bling sinyuki, sina mvuto sitoki smart

Mrefu sio mfupi, bora ningekuwa saizi ya kati

Au sikuvutii, ndio maana hunipi uthamani

Kioja ndani ya jamii, na kwanza haturandani

Pia hujisikii, kuwa na kapuku kama mimi

Ambae mswaki situmii, sina hadhi ya kunyonya ulimi

Au mpaka mavumba, ndo mapenzi yashamiri

Hata suala la unyumba, mpaka kwa muda ufikiri

Au umepata mchumba, mjanja tena tajiri

Sio mimi katumba, mla ganja nisie na dili

Au sijui mahaba, kitandani sikuridhishi

Sikuombi nakaba, tendo la ndoa kwa ubishi

Siwezi kubembeleza, kiupole ama siimbishi

Au sijui kuchombeza, kileleni sikufikishi

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au sababu mi wa bara, mwenzangu unatoka pwani

Ndo maana unaniona fala, wakati wa mambo flani

Niambie, ka siko imara kasoro weka hadharani

Nipunguze papara, nichezapo mechi uwanjani

Au umechoka ukonga, tukaishi kimara

Milima ya kitonga au safu za usagara

Hutaki niendeshe honda, unataka nidrive vitara

Haupendi samaki ng’onda, nikupe sato sangara

Au niache muziki, tushinde tu chumbani

Ufurahi kumuona nikki hakiwa hatoki ndani

Tukiandamwa na dhiki tutaishi maisha gani

Kiundani haifikiriki ya mbele mbona hutazami

Au sio nyota yangu, nimepiga wrong number

Nakuforce uwe wangu, damu zetu haziendi sambamba

Nimekuja na mkuki nataka kuutoboa mwamba

Wakati wenye bunduki mbele yako wameshindwa tamba

Wivu umezidi upendo ni uvivu zaidi ya vitendo

Kila siku lawama na kunizushia skendo

Kama hunitaki ni vema uniweke wazi

Nijue nitambue kwani mademu wapo shazi

Kwani vipi unayofanya mbona mchizi sikuelewi

Haki yangu hunipi hata mahitaji yangu ya msingi sipewi

Kwani vipi unayofanya mbona mchizi sikuelewi

Haki yangu hunipi hata mahitaji yangu ya msingi sipewi

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au kisa msanii unahisi wenzako watakupiku

Mchizi huniaminii, show za mkoa ama za usiku

Nitakupa HIV sababu mchapa nje ya ndoa

Changu sidime milupo vicheche makabakoa

Au labda situngi, mashairi ya kukusifu

Sina sony sifungi, hisia zangu kwako hafifu

Natafuna mirungi, uswahilini ni mtu wa tifu

Lakini sijidungi, huo ndo ukweli yakinifu

Au labda umenichoka, ila hutaki kunieleza

Kwamba nikki ondoka, me nimeshapata mwenza

Mbona mchizi nang’oka, kisha michongo nasebenza

Kwani mapenzi ya nyoka, si kwenye majani kuteleza

Hivi ni hiyari yako, au ulinipenda kwa shinikizo

Kutoka kwa rafiki zako, uliokuwa nao enzi hizo

Si ulifuata medako na wekundu wa mfululizo

Utizime hazma yako, pesa zangu zimekwenda likizo

Fikra ndani ya medula tamati picha samati

Wa chuya umeula eeh si hunipendi kwa dhati

Binadamu kwa sura, kiundani una roho ya nyati

Unanichezea sangula, hujui unanipotezea wakati

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

Au mama kukufuata ninakuchosha

Au tena we unaomba usinione tena

By Mugizi Jr.

Similar Songs

+

      -   or   -

      -   or   -

      NG +234

          Please Select A Playlist

          Add New Playlist

          Share on

          Embed: Love & Light EP

          Custom Size :

          • Default
          • Desktop(300*600)
          • Mobile(300*250)

          Type :

          • HTML/HTML5 (WordPress Supported)
          Get Boomplay Premium
          for
          Payment Method
          Pay With
            Review and pay
            Order Date
            Payment Method
            Due Today
            Flutterwave
              Subscription Successful

              Congratulations! You have successfully activated Boomplay 1 Month Premium.

              Now you have access to all the features of Boomplay App.
              Payment Failed

              Please check your balance and then try again.

              You'll lose your subscription if we don't have a working payment method for your account, so please check your payment details.
              Need help? Contact Boomplay Subscription Support.
              Payment Processing...
              10 s

              Payment is being processed by . Please wait while the order is being comfirmed.

              Payment Processing
              Your order is processing, and it may take up to a few days for the service provider to handle your payment. Please kindly stay tuned and check your order status in ‘User Center’.
              About Order Status