I am Free (Live) ft. Najma Juma & Joyce Gerald Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2021
Lyrics
Nakumbuka nikisimama mbele ya kanisa
Nikiungama dhambi maarufu
Nilihisi nimewashtua watu
Wengine naamini niliwakwaza
Moyoni nataabika kunyamaza
Sauti za hukumu na shutumu kutonyamaza
Naanzaje kutangaza tena Ufalme wa Mungu?
Je, mimi ni mwana wa Mungu?
Nilikosa majibu
Moyo wangu ulizama kwenye giza
Uchungu ulopitiliza
Miguu yangu haina nguvu
Sina hamu wala hamasa na kitu
Nikaendelea na siku
Ni nani awezaye kukomboa nafsi ilohukumiwa?
Maana ni kama mtu aliye mfu
Mshahara wa dhambi ni mauti
Je, dhambi ni nini hata ujitwike kwa ajili yangu?
Umejitwika dhambi mwilini mwako, ukaaibishwa
Ukapigwa hatimaye kifo
Hii ndio namna dhambi inatesa
Lakini ukaishinda, na kifo ukakishinda
Ukashuka chini hata kwa waliokufa
Wewe mwenye ujuzi wa miisho ya dunia, ukajitwika hata dhambi za wasio hai
Uliye na uwezo wa kusamehe dhambi
Ulimwambia yule mwanamke aende zake, wakati wa aibu, na kupigwa mawe
Kweli umekuja kuiondoa dhambi, na upendo wako ni ufunguo
Nikawa mbali na watu, mbali na urafiki
Nilijiona mpweke hata wakiwa karibu
Niliuchukia usiku
Nilipoteza thamani ya siku
Naamka asubuhi lakini bado ni usiku
Ndani yangu hakuna nguvu
Akili imechoshwa na sauti za kujihukumu
Lakini hukuniacha
Ulisema nami kama upepo, ukanikumbusha bado upo
Hata nilipodhani nimekosea mpaka mwisho
Kama mwana mpotevu hujaacha kunionesha fadhili zako
Kwa miali ya jua dirishani mwangu ulisema nami
Ukanikumbusha rehema zako ni mpya kila asubuhi
Mpaka nivyopojua ulikuja kwa sababu hii
Kuniondolea hukumu, kunipa uhuru
Sikuona wala sikutambua mpaka nilivyoonja pendo lako
Hukumu hutuweka mbali na Mungu, roho wa uzima hutupa uzima
Na wala kwake hakuna hukumu
Kama hii stori ni yako, unadhani umekosea mpaka mwisho
Umekosa matumaini, umejihukumu na kujiadhibu
Unajiuliza kama watakuelewa
Unahisi watu watakutenga
Unawaza itakuwaje kama wakigundua
Ujue ukweli huu na uwe huru
Roho wa uzima ametuweka huru juu ya utumwa wa dhambi
Mimi na wewe tumeondolewa dhambi
Hatuna sababu ya kujihukumu, kwa maana Mungu hatuhukumu
Tazama upendo huu na ukajipende namna hii
Ni yeye alikupenda hata kabla hujasema ndio
Anayekujua kabla ya misingi ya ulimwengu kuwekwa
Anayekuombea usiku na mchana
Ni yeye anajua nia ya moyo wako
Ni yeye anayekuita mwana
Simama na uangaze shujaa
Simama na utangaze zake rehema
Kwa maana umesamehewa
Wewe ni shahidi wa mataifa
Kwa ushuhuda wako unaangusha ufalme wa giza
Tazama siku za utukufu zi hapa
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free
I am free
So free
Am free