Loading...

Download
  • Genre:Afrobeats
  • Year of Release:2020

Lyrics

Kaka Tuchat - Rostam (TZ)

...

(Tongwe Records)


Oooii naona mtandao unakatika

Upo kimya sana mkato au kunde imevunjika

Na mtanyooka roundi hii

Na hivi huwezi bila mimi?


Najikuta Jay Z oya unarudi lini?

Kaka huku wamefunga mipaka

Ila tiketi nilikata nirudi kabla ya pasaka

Rudi ugeuze kisu sio

Mwana wa kulitafuta mwana wa kulipata

Round hii sio nunio, daraja la mpasu





Kumekucha hivi saa ngapi huko nipe takwimu

Nimeamka nishaweka bundle namngoja Umi mwalimu

Anapambana yule dada

Tanga nimewavulia kofia wametoa sanitizer za iliki

Yaani ukipaka unanukia


Hehehe Corona nishai yaani Bongo kila mtu daktari

Masai kachemsha maji ya mpapai kanywa na sukari

Guza hadi maski wanafua sijui ni nani kawafundisha

Huku kuna dada kajifukiza mashetani kayapandisha


Tueke siasa kando unajua uchumi unashuka

Sio Bongo tu hadi ng'ambo watu wamefunga maduka

Hapa nawaza pesa ya bango benki walokopa wanajuta

Tukisema tukae ndani na hii njaa si tutakufa


Hali inatisha na umasikini, tunaoumia ni sisi

Yaani bora ufe kwa Ukimwi angalau utaandika urithi

Kwa iyo hamna bata, sio kidimbwi sio tipsi

Kaka madanga yamekata so hazitimbi hizo piece


Bwana wa mabwana Mungu wa miungu

Alpha na Omega nani kama wewe

Bwana wa mabwana Mungu wa miungu

Alpha na Omega nani kama wewe


Hivi unakaa jimbo gani au Marekani

Unajikinga vipi maana vifo vingi hadi siamini (Mmmh)

Au umesharudi ipo zako Horohoro nini

We bwana hebu niache mi nimeze chloroquine


Umenikumbusha kweli Chloroquine ni dawa?

Bado inafanyiwa uchunguzi ila haijadhibitishwa

Ingawa ukinywa haitohatarisha ndio maana bado wanaigawa

Mi ninakunywa maana nilishika uso kabla ya kunawa


Eti unaweza ukawa nayo na usionyeshe dalili?

Ewaah! Uko sahihi, na kingine kuhusu hili ni kwamba

Mgonjwa wa Corona unaweza usimtambue kwa macho

So mtu yeyote unayemuona mpe mita mbili toka kwako


Na hiko kiVansileka ndo kinini baba wawili?

Ni ventilator, ni mashine ka mapafu ya nje ya mwili

Mmmh sijaelewa hebu nieleweshe kuhusu hili

Naskia vinauzwa ghali basi viwe vingi Muhimbili


Okay, kirusi cha Corona kinashambulia mapafu

Ndipo zinaanza homa, kifua alafu

Unashindwa kupumua na mwili unahitaji tafu

Ventilator huingiza hewa na kuitoa iliyo chafu


Tuepuke mikusanyiko ikibidi tukae ndani

Tumeambiwa tujifukize hivi ni dawa unadhani?

Ngoja kwanza, hivi fumigation (Mmmmh mmh)

Baba ile inaua mende eti (Hahaha wacha utani)


Bwana wa mabwana Mungu wa miungu

Alpha na Omega nani kama wewe

Bwana wa mabwana Mungu wa miungu

Alpha na Omega nani kama wewe


Maisha ya upweke yanasumbua ila siku zinapita

Yule mkewe itunze pete

Mtayamaliza na uhakika kaka

Ila hatua dua haina haja ya kusikitika


Ila navyokujua hujazini miezi sita?

Kiukweli mi mwaminifu ingawa jogoo anawika

Mama Ivan mbabaifu haku-cheat una uhakika?

Kuna mchezaji wa Yanga namwona anapita pita


Nitamkata kata mapanga yaani namuua na namzika

Oyaah wape nyumbani basi pesa ya matumizi

Kaka nitoe wapi na show hakuna siku hizi?

Hali imekuwa ngumu hakuna pesa kila kona


Kila mtu unayemdai naye anasingizia Corona

Mbona sasa wanafunga shule na vyuo alafu bar hawafungi

Mzazi atamlindaja mtoto na akirudi yuko tungu?

Polisi India wanapiga watu wakisongamana


Wao barakoa hawana, jua defender wamebanana

Sasa wanatukusanya kutuambia tusikusanyike

Ila wauguzi wanajitoa sana, dah Mungu awalipe

Wapinzani mnatangaza vifo walopona hamwatangazi


Ah-ah wanasema wangeweka takwimu za wazi ingekuwa kizazi

Kwa hivyo lockdown hakuna alafu umeona text niliyotuma?

Ipi kwenye group mbona inbox hakuna?

Ah naskia (Nini?) koyuzeka mbochi

Maana uliko uliko usiongee sana inatosha

Hadi papai lina Corona dah (Kaka tuchati)

Mmmh ina mbuzi vipi? (Eeh eh kaka tuchati)

Mwili umekufa ngazi (Kaka tuchati)

Poa mwanangu tuendelee kujifukiza


(Tongwe Records, Bin Laden)

+

      -   or   -

      -   or   -

      NG +234

          Please Select A Playlist

          Add New Playlist

          Share on

          Embed: Love & Light EP

          Custom Size :

          • Default
          • Desktop(300*600)
          • Mobile(300*250)

          Type :

          • HTML/HTML5 (WordPress Supported)
          Get Boomplay Premium
          for
          Payment Method
          Pay With
            Review and pay
            Order Date
            Payment Method
            Due Today
            Flutterwave
              Subscription Successful

              Congratulations! You have successfully activated Boomplay 1 Month Premium.

              Now you have access to all the features of Boomplay App.
              Payment Failed

              Please check your balance and then try again.

              You'll lose your subscription if we don't have a working payment method for your account, so please check your payment details.
              Need help? Contact Boomplay Subscription Support.
              Payment Processing...
              10 s

              Payment is being processed by . Please wait while the order is being comfirmed.

              Payment Processing
              Your order is processing, and it may take up to a few days for the service provider to handle your payment. Please kindly stay tuned and check your order status in ‘User Center’.
              About Order Status