Ni Tabibu Wa Karibu Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2013
Lyrics
Ni Tabibu Wa Karibu - Fanuel Sedekia
...
TENZI No7.
NI TABIBU WA KARIBU
1. Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.
Imbeni, malaika,
Sifa za Yesu Bwana;
Pweke limetukuka
Jina lake Yesu.
2. Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.
3. Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twenendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.
4. Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.
5. Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.
6. Na vijana wote tena,
Wampendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.
Shared from Tenzi za Rohoni app.
Click this link to download *goo.gl/9HNM1M