Hatua Lyrics
- Genre:Trap
- Year of Release:2023
Lyrics
Kwa uwezo wa Mungu niko hapa mi nafanya yangu, yangu, yangu,yangu,
Siwapi nafasi wavunja moyo kwangu, katu,katu, katu,
Niko na nguvu toka juu na baraka za wazazi wangu,
Sina hofu ndani yangu,
Sina hofu ndani yangu,
Nina nguvu ndani yangu,
Nina nguvu kubwa kwangu,
Hodi hodi bongo fleva, nahitaji namba nahitaji cheza,
Nahitaji taji nahitaji kiti, nahitaji heshima nahitaji fedha,
Nahitaji watu niwapige pindi, sio chawa maku,
Nahitaji vazi litoke juu, siimbi tu na rap,
Niwapo mi ni amani tu ni raha tu ni upendo tu,
Ndani yangu miujuzi tu mi kung fu ya hali ya juu,
Mchezo huu naumudu mi naufanya nitakavyo tu,
Naufanya freshi ka ya Fid freshi, nauweka juu ka ya Nenga puuh,
Nawaeka huru walionyimwa keki ke keki ya taifa keki,
Flow steki haina mfupa flow zangu ndo hiyo steki,
Nimepikwa kwa kila mechi kwakila mada nazivunja benki,
Kwa kila neno nazishtua beki naifanya jamii inifaidi keki,
Baraka za Mungu na wazazi ndizo zinanipandisha ngazi,
Baraka za Mungu na wazazi ndizo zinanipandisha ngazi,
(Asante)
Niko na nguvu ya Mungu ndani yangu niko na nguvu yakuifanya bongo iwe babalao,
Niko na dawa ya sumu dawa ya pumu dawa ya gonjwa litusumbualo ,
(Asante)
Niko na maji ya uzima maji ya mtima usikose lile upendalo,
Niko na nguvu ya kweli meno ya chuma kutafuma lile lishindikanalo,
Asante
Asante
Msije kuhisi nimekuja kujaribu,
Mkaacha kunipa mkono mniadhibu,
Nishindwe kufika swali kulijibu,
Tuishi ka wale wa sizitaki hizi mbivu,
Haya maji nshayavulia nguo lazima niyaoge,
Hii vita muhimu kwangu ka mlevi akiiona pombe,
Hili shamba roho yangu lazima nililinde lote,
Sina hofu na waleta hofu nna hofu ya Mungu sio kobe,
Na hofu ya Mungu imenipa nguvu niite komandoo,
Siimbi uchafu siupambi uchafu mi nikioo,
Kwahiyo naimba vya faida kwa taifa,
Maarifa kwa taifa kuyagawa kwangu mimi uwakika,
Fanya kunifuata kule insta, facebook, youtube ,kule twitter,
Unapopita usiache penda nachopika usiache sambaza nilichopika,
Mi mpishi mpishi safi,
Mi mwalimu mwalimu bora mi kiongozi kiongozi safi,
Baraka za Mungu na wazazi ndizo zinanipandisha ngazi,
Baraka za Mungu na wazazi ndizo zinanipandisha ngazi,
Asante
Niko na nguvu ya Mungu ndani yangu niko na nguvu ya kuifanya bongo iwe babalao,
Niko na dawa ya sumu dawa ya pumu dawa ya gonjwa litusumbualo,
Asante
Niko na maji ya uzima maji ya mtima usikose lile upendalo,
Niko na nguvu ya kweli meno ya chuma kutafuna lile lishindikanalo,
Asante
Asante.