Loading...

Download
  • Genre:Hip Hop & Rap
  • Year of Release:2022

Lyrics

Sina tafiti yoyote ila nabonga kwa ujasiri/

Kwamba wote mnajua kuwa kukopa ni nini/

Na ili mada iwe tamu uskute wote mnadaiwa hapa/

Mnabisha? Mbona wote hamuitikii sasa/

Iza, hiyo ni commercial break/

Haya wote turudini katika mada yetu hii/

Kwanza jiulize kwa nini unakopa/

Jishauri au omba ushauri kabla ya kutoka/

Jua utafanya nini kisha ukakope/

Sio ukope ndo utajua kichwa matope/

Na tafuta mikopo yenye riba nafuu/

Watu wengi wameumizwa kwenye riba za juu/

Kopa kiasi unachoweza kurudisha/

Acha tamaa sifuri unazoongeza utazilipa/

Na Hela nyingi usikope kuanzisha biashara/

Mkopo ni wa kuimarisha biashara/

Hiyo hela inabidi izunguke ili izae/

Ili deni lipunguzwe hawajakupa Ili ikae/

Na achana na biashara za kupata majaliwa/

Kuwa fasta na ambazo ukizifanya uhakika/

Kuwa makini sana na dhamana/

Usije poteza vitu vya thamani na vya maana/

Kama mali sana sana/

Nini samani, nyumba zinauzwa mchana mchana/


Mikopo ina ubaridi na joto la maana/

Mikopo ina faida na mikopo ina hasara/

Yani ina pande mbili ka sarafu/

Kwa hiyo cheza kwa akili acha rafu/

Ukiliwazwa na matunda ya ukimaliza kulipa/

Waza na za hatua za ukishindwa kulipa/

Kuwa makini na mikopo tuliza akili kwa mikopo/

Kuna utajiri kwa mikopo na umaskini kwa mikopo/


Mara tu unapopewa usizuzuke na pesa/

Sababu za kuombea uzikumbuke mapema/

Mzee wangu acha kukopa ukaponde raha/

Kula nyama choma kugonga mapombe bar/

Na mamdogo unauchubua ka huskii/

Usitegemee mkopo kununua waksi/

Au Kupika kupakua mahanjumati/

Kulumbua ili kuwaumiza pua majirani/

Mikopo yenye faida ni ile inayokimbiza lengo/

Yenye tija ile Inayotimiza lengo/

Ile ambayo ikiisha inakuacha umesogea/

Piga mahesabu uone umepata umepotea/

Kila ukitaka kulala kumbuka unadaiwa/

Hii itafanya uwahi kuamka na hasira/

Kudamka na dhamira ya kutafuta ngawira/

Kungachamka ili mifuko iweze umuka ka ina hamira/

Ka malipo ni ya awamu aisee acha mchezo/

Zingatia sana tarehe ya marejesho/

Ili kuepuka fine au adhabu/

Usilale au ukae uandae na sababu/

Kumbuka fine kama utumbo itakujazia nzi/

Utachelewa kumaliza itakupunguzia speed/

Ukijiskia uvivu kukomaa hata kidogo/

Rudi Kasome tena masharti ya mkopo/


Mikopo ina ubaridi na joto la maana/

Mikopo ina faida na mikopo ina hasara/

Yani ina pande mbili ka sarafu/

Kwa hiyo cheza kwa akili acha rafu/

Ukiliwazwa na matunda ya ukimaliza kulipa/

Waza na za hatua za ukishindwa kulipa/

Kuwa makini na mikopo tuliza akili kwa mikopo/

Kuna utajiri kwa mikopo na umaskini kwa mikopo/


Yeah, Wazoefu wanakwambia siku zote/

Kama hakuna ulazima usikope/

Maana Kukopa harusi ila kulipa matanga/

Kukopa ni nuksi acha kuita majanga/

Unaambiwa usikope kisa flani amekopa/

Au umetamanishwa na tangazo ukanyooka/

Ule ulimi mtamu wa afisa mikopo/

Usikuchanganye maana akibadilika ni nyoko/

Hujaskia mtu amekimbizwa madeni/

Anaishi kwa mashaka anajificha na hahemi/

Heh!! Akiskia hodi tu presha/

Hata usingizi hauoni anakesha/

Unacheza. Watu wanafilisiwa kutwa kucha/

Wapo waliokimbia familia wakazisusa/

Wapo waliopata magonjwa mpaka sasa hawajapona/

Waliobahatika kurudi wengi wao wamekoma/

Mikopo inatesa saa zingine inaua/

Sio maskini tu hata matajiri wanajuta/

Ila ukituliza kichwa na ukaenda na muda/

Ukajifunga kabisa mbona utayapenda matunda/

Jifunze kwa wale walioinuka kwa mikopo/

Jifunze zaidi kwa waliokutwa na mikopo/

Ningekwambia kuhusu Serikali na mikopo/

Ila kuweka roho rehani ndio sitakagi hiyo mikopo/.

More Lyrics from Micshariki Africa Songs

Similar Songs

+

      -   or   -

      -   or   -

      NG +234

          Please Select A Playlist

          Add New Playlist

          Share on

          Embed: Love & Light EP

          Custom Size :

          • Default
          • Desktop(300*600)
          • Mobile(300*250)

          Type :

          • HTML/HTML5 (WordPress Supported)
          Get Boomplay Premium
          for
          Payment Method
          Pay With
            Review and pay
            Order Date
            Payment Method
            Due Today
            Flutterwave
              Subscription Successful

              Congratulations! You have successfully activated Boomplay 1 Month Premium.

              Now you have access to all the features of Boomplay App.
              Payment Failed

              Please check your balance and then try again.

              You'll lose your subscription if we don't have a working payment method for your account, so please check your payment details.
              Need help? Contact Boomplay Subscription Support.
              Payment Processing...
              10 s

              Payment is being processed by . Please wait while the order is being comfirmed.

              Payment Processing
              Your order is processing, and it may take up to a few days for the service provider to handle your payment. Please kindly stay tuned and check your order status in ‘User Center’.
              About Order Status