Hayakuwa Mapenzi Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2009
Lyrics
Hayakuwa Mapenzi - Sugu (TZ)
...
Yeah
namnagani mchumba sio kwamba nina hasira inabidi tuongee tu sio au sio, maana ake long time atujaongea sio na hata sijui nini kilitokea hasa mimi labda wewe unajua!! lakini mimi sijui, mimi sijui,
Nikama nyimbo ya mapenzi, nikama nyimbo ya penzi,
(Yeah) Yale hayakuwa mapenzi, yale hayakuwa mapeenzi,
Mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi,
Yale hayakuwa mapeenzi, oohh yale hayakuwa mapeenzi,
mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi
Naamini nilikupenda na ndio maana sikupenda ulipo amua kwenda, na mpaka leo najiuliza sijui ningefanya nini ndo nisinge kupoteza, nilifanya kilakitu nilicho weza,
Kumbuka nimara ngapi mtu mzima ulimliza (choozi),
Sikutaka tuachane tulikaa muda mrefu, tulijuana kwa mapana na marefu, na tulifurahia pamoja muziki ulipo nipa umaarufu,
Nami sikuvimba kichwa kwani mapenzi yangu kwako yaliongezeka maradufu, nawe herufi ya jina langu uliliweka kwenye kidani cha mkufu,
na niwewe tu na mama ndo hamkuniita mr. Two bali Joseph,
Nilijiona dume mimi maranyingi uliposema hakuna penzi kama ninalokupa mimi,
Ukaapa kuishi nami na ikibidi kufa nami, lakini ukabadirika na siamini kama leo haupo nami.
Yale hayakuwa mapeenzi, yale hayakuwa mapeenzi, mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi,
Yale hayakuwa mapeenzi, oohh yale hayakuwa mapeenzi,
Mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi.
Uliondoka kam utani, yani nilikua penzini ghafla ukaniacha gizani,
Napita mitaani mawazo tele kichwani, washkaji wananiuliza shemeji hajambo nyumbani, nitawajibu kitu gani?? Nikisema tumeachana nitawapa sababu gani? (Hhaaa)
Wee uliondoka tu, nampaka leo katu, hata hujasema kitu,
Nami sitaki kufuata yanayosemwa na watu,
wanasema wazaziwako waliona kwangu eti future hamna kitu (aahhh)
Siwezi kuwapa lawama kwakukutakia mema story za maisha yangu nilikueleza mapema,
Sikupenda kutokuendelea kusoma,
Baba alipofariki ilibidi nimtunze mama, nazidi ni kuhakikisha wadogo zangu wanasoma, hainanoma, maisha bado yatasimama na hatuwezi kurudisha wakati nyuma, NOO.
Yale hayakuwa mapeenzi, yale hayakuwa mapeenzi, mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi,
Yale hayakuwa mapeenzi, oohh yale hayakuwa mapeenzi, mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi,
Niliamini kilicho fuata ni uchumba,
daima penzi langu kwako halikuyumba, ulipata matatizo madactari waliposema ungeweza kuwa mgumba,
bado nilikuwa tayari kwani maisha yetu ya mbele mi nilimuachia Muumba,
Mungu ndiye anaye mpangia kila mmoja, wangapi walizaa watoto na wote wakawa mateja,
Najapo sasa uko mbali, bado nakumbuka dinner kwenye hotel kalikali, sometimes pekeyetu na sometimes na washikaji mbalimbali, mambo yalivyokuwa mazuri, nilikua mwanamuziki tu sikuwa mafanyabiashara,
na maranyingi mishiko niliipata kwenye ziara,
Kumbuka nilipiga show toka Arusha mpaka mtwara, yote ni kusaka hela,
Na kwapenzi nilijitahidi kulienzi,
Kilicho nisikitisha kwako hayakuwa mapenzi,
Yale hayakuwa mapeenzi, yale hayakuwa mapeenzi, mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi,
Yale hayakuwa mapeenzi, oohh yale hayakuwa mapeenzi, mbona nilikupa penzi lakini nashangaa ukashindwa kulienzi.
Music!!!!!!!!!!!!!!!