Jeraha Lyrics
- Genre:Bongo Flava
- Year of Release:2021
Lyrics
Jeraha - Ziddy Value
...
Sina budi kuridia, nizoee taratibu nijifosi
ingawa moyo ndo vile
Kadi yako imefika, naskia umempata mwarabu unajiposti
Ntakuja kwenye sherehe
Na kile kioo ulichokua unatumia, kujitazama
Ntakitunza, ibaki kama kumbukumbu
Vile roho ya choyo sjaumbiwa, hakunifunza mama
Hivyo ningependa usiache pokea salam zangu
Sawa, ntakuita shemeji, na maua kama zawadi
Macho yatantoka maji, ntajifuta kujifariji
'naposhuka mvua za radi, peke yangu ntahisi baridi
Nnapokua bored, na moyoni bado litasumbuaa
Ooh yeah
Jeraha, (kidonda kibichi umekisugua)
Jeraha (moyo umentapakaa damu)
Jeraha (jeraha maradhi ya moyo)
Jeraha (umeutenganisha mfupa na shahamu)
Ona umenshushia dho'hali, hali ya kuwa bado yangu hatima
Umeniacha dhil'hali, licha ya kukutunzia heshima
Si ulisema tuanze safari, hutonishusha kwa njia na
Vile penzi mfano wa bahati, nami sikuelea nkazama
Umenipa wakati mgumu, umeutoboa mshipa wa faraja
Ila niape kutolaumu, jambo la ndoa kwa Mungu ni ibada
Ntakuita shemeji, na maua kama zawadi
Macho yatantoka maji, ntajifuta kujifariji
'naposhuka mvua za radi, peke yangu ntahisi baridi
Nnapokua bored, na moyoni bado litasumbuaa
Ooh yeah
Jeraha, (kidonda kibichi umekisugua)
Jeraha (moyo umentapakaa damu)
Jeraha (jeraha maradhi ya moyo)
Jeraha (umeutenganisha mfupa na shahamu)