Mv Bukoba Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2015
Lyrics
Mv Bukoba - Hedaru Central Church SDA Choir
...
Ilikuwa tarehe ishirini
na moja mwezi ule wa 5
mwaka elfu moja mia tisa tisini na sita ndugu zetu wapendwa
waliianza safari yao
katika usiku wa manane
walipokaribia kufika kulikuwa kumeanza kupambazuka alfajiri
na mataa ya mji wa mwanza-alfajiri
yalishaanza kuonekana - alfajiri
wasafiri wote wakawa na tumaini kuwa watafika salama,
wengine walilala usingizi
na wengine walikunywa pombe,
wengine walifikiria kuuza biashara zao wakifika mwanza.
wengine walilala usingizi
na wengine walikunywa pombe
wengine walifikiria kuuza biashara zao wakifika mwanza.
Ndipo tufani ikatokea,
meli ikapigwa na mawimbi
ikaanza kuyumba na kuyachota maji na mwisho ikaanza kuzama,
watu wakaangua vilio,
wakiuhitaji msaada,
zikafika boti za wavuvi kuwasaidia lakini hazikutosha kabisa,
waliookolewa wachache - Kabisaa
wengi wakafa ndani ya maji - Kabisaa
waliokufa ni masikini na matajiri wenye vitu vyenye thamani,
walijaribu kutoa fedha
ili wapate kuokolewa,
hawakupata mtu wa kuzipokea wakafa nazo kwenye mifuko.
walijaribu kutoa fedha
ili wapate kuokolewa,
hawakupata mtu wa kuzipokea wakafa nazo kwenye mifuko.
Na dunia hii
nayo ni sawa kabisa,
na meli inayosafiri baharini,
tumeshasafiri usiku wa manane
na alfajiri nayo imekaribia,
tumeshaiona bandari sio mbali,
lakini bahari nayo imeshachafuka,
na safari yetu imeshakuwa na mashaka
kwani chombo chetu kinapigwa na mawimbi sana.
Wewe ndugu!
ingia ndani ya boti ya yesu-ili
Ili uokolewe na ajali- Kwani
Kwani boti yake haina gharama yoyote.
Wewe ndugu!
Fanya uamuzi leo twende-ili
Ili tukaishi na mwokozi - ndugu
Katika nchi mpya mwokozi katungojea
Sasa njoo ndugu
tukatawale
Tukafurahie
mji wa raha
Tukaishi na yesu
Kule mbinguni
Nawe Baba
njoo leo tukatawale
Tukafurahie mji wa raha
Tukaishi na yesu
Kule mbinguni
Nawe Mama
njoo leo tukatawale
Tukafurahie mji wa raha
Tukaishi na yesu
Kule mbinguni
Nawe Kaka
njoo leo
tukatawale
Tukafurahie
mji wa raha
Tukaishi na yesu
Kule mbinguni
Nawe Dada
njoo leo tukatawale
Tukafurahie mji wa raha
Tukaishi na yesu
Kule mbinguni