Utukuzwe Ewe Baba Lyrics
- Genre:Afrobeats
- Year of Release:2019
Lyrics
Utukuzwe Ewe Baba - Tumshangilie Bwana
...
Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya
Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya
Utukuzwe - utukuzwe
Baba Muumba ulimwengu - aleluya
Tumepokea mkate, mazao ya mashamba, aleluya
Ndio alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya
Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya
Jalie uwe kwetu, chakula cha uzima, aleluya
Zawadi ya divai, kutoka mzabibu, aleluya
Ndiyo alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya
Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya
Jalie iwe kwetu, kinywaji cha kiroho, aleluya
Sifa kwako ee Mungu uliyetuchagua, aleluya
Shukrani kwako Baba, kwa kutulisha sisi, aleluya
Kwa pendo na fadhili, umetufurahisha, aleluya
Ukatufikisha kwa sherehe yetu leo, aleluya
Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa, aleluya
Na utukufu wako na kwa mafaa yako, aleluya