Ukoloni (feat. Nash Mc) Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2021
Lyrics
Ukoloni (feat. Nash Mc) - Bwajah & Pato
...
Naililia Africa Siasa za chuki
Kila napopita nakasirika napoona Damu nyeusi inamwagika
Hali inatisha usilewe Madaraka Utaanzisha vita
Waachie wenzio muda wako unapokwisha au umenunuliwa na Mabeberu unalinda maslahi Yao
Hii ni mpaka lini tuwasujudie wao
Umaskini unaongezeka na mali zipo kibao
Aah Tumestuka kumbe ni wenzenu mnatukandamiza na mnakula pekeyenu
Uhuru wa bendera umetawala bara Zima
Mwananchi yupo hoi amezama kwenye kina (Kina kirefu hatarudi zaidi ya Jina)
Njia za uchumi wamekamata wachina
Wamarekani, Waingereza Wimawima
Wajeumani, Wafaransa wote machopima
Mwafrika zinduka amka Kaa wima
Ukoloni mamboleo ndani ya System (System System)
Ukoloni mamboleo ndani ya System
(System wee System)
Hii system ni zaidi ya unavyowaza
Mashairi chambua Kwa mwendo wa kukaza
Ukoloni mambo Leo ndani ya System
(System System)
Ukoloni mambo Leo ndani ya System
Hii system ni zaidi unavyowaza
Mashairi chambua Kwa mwendo wa kukaza
Napiga hatua kwenye mawazo Kuna mengi ya kusema sasa uliza Matangazo Matatizo mitaani hakuna Amani Kaa
Tunaishi kivikwazo nafikiria lini maendeleo yatakuja fika Afrika
Labda mpaka ufisadi utakapokwisha Ukoloni mkongwe wa weupe bado upo juu ya system na sisi ndio Victims ndani ya ukoloni wa weusi kwenye hii system
Njaa, Demokrasia yatupeleka pabaya ukweli ukisemwa watakupangia mabaya Vipi kura yako iwe silaha yako wakati serikali haijali maisha yako,
Katiba kama kibaka kuna wakati haitapendeka ikizuiwa ya kuitaka nani atasalimika Chama sas ni Sanaa wajinga kununuliwa Kwa maamuzi ni Sanaa Uislamu unatakiwa mwizi anayetuibia wenyewe tunawajua
Jobless waliokuwa ndo viongozi huwachagua Government to shine the Syllabus we need black to be twice free massive
Elimu, Tamaduni na Historia za Afrika
Ukoloni mamboleo ndani ya System (System System)
Ukoloni mamboleo ndani ya System
(System wee System)
Hii system ni zaidi ya unavyowaza
Mashairi chambua Kwa mwendo wa kukaza
Ukoloni mamboleo ndani ya System
(System System)
Ukoloni mamboleo ndani ya System system
Hii system ni zaidi ya unavyowaza
Mashairi chambua Kwa mwendo wa kukaza
Afrika zinduka Leo hii ndo kesho Ulioisema jana mbona ishafika inuka Eyoo
Juhudi za maendeleo kimaksudi wenye vyeo wamebana sa tazama Utawala wa kimabavu unaoshamiri Kwa mtutu wa Bunduki we umelala huku hawana Utu ka mamluki
Hakika katika msiba ndo wanatafuta sifa Katiba wanabadilisha ili wajipe nyazifa
Raia wanataabika hamna tena Uzalendo ni Ufisadi na magendo huku Taifa likifa
Huo ndo ubepari mjukuu wa Demokrasia tayari ka sikukuu elewa msemo na Hisia "Ushikwapo Shikamana" ni mistari ya Elimu haitashika maana
Ukoloni mamboleo ndani ya System (system Yeeeah)
Ukoloni mamboleo ndani ya System (System System)
Ukoloni mamboleo ndani ya System
(System wee System)
Hii system ni zaidi ya unavyowaza
Mashairi chambua Kwa mwendo wa kukaza
Ukoloni mambo leo ndani ya System
(System System)
Ukoloni mambo leo ndani ya System system
Hii system ni zaidi unavyowaza
Mashairi chambua Kwa mwendo wa kukaza
(Lyrics by AT Man Don )