Usinipangie Lyrics
- Genre:Bongo Flava
- Year of Release:2020
Lyrics
Usinipangie - Jacan
...
Beat intro......
Kimambo on the beat...
wazazi walitaka niwe msomi, wakiamini kazi ni ofisini.
wife anataka niwe baba bora, nikichelewa kurudi ni msala.
wakati nipo kwenye mishe za hela, anahisi nadanga na navaa madela
Tungi kiasi usinipangie, matumizi kiasi najua mie.
Eti nimwendo kasi niwapunguzie, maneno kiasi msinijazie
Maswali mengi huwa sijibu mie
Mipango mingi hainihusu mie.
Hoja za msingi pelekeni bungeni,
akili nyingi pelekeni shuleni,
Mawazo mengi msiniwazie mimi
Vidole vingi onyesheni mbinguni.
*chorus*
Wasinipangie.
Wasinihofie
Wasinichukie
Nafanya navyotaka mie. ×2
verse ii
Nigaz wanapanga panga sanaa.
Mamanzi wanachonga chonga sana
Nimefanya kipi juzi jana
Kwangu issue sio issue sana
Nikikukwaza am sorry sana
Kujikweza sijuagi bhana
Kujipendekeza utangoja sana
Kujiongeza kawaida sana
Kila kitu wanataka kucomment..
nikifanya eti nifanye vipi,
hata kutoka eti nitoke na yupi
Hata kuvaa eti nivae vipi..?
Usinijudge please, usinigasi
Usinilike pia sio kesi
Maisha yako less tupeane nafasi
Yanini kushare mpaka mambo binafsi.
Hoja za msingi pelekeni bungeni,
akili nyingi pelekeni shuleni,
Mawazo mengi msiniwazie mimi
Vidole vingi onyesheni mbinguni.
*chorus*
Wasinipangie.
Wasinihofie
Wasinichukie
Nafanya navyotaka mie. ×3
beat outro.....