Kekundu Lyrics
- Genre:Afrobeats
- Year of Release:2013
Lyrics
Kekundu - AIC Makongoro Vijana Choir
...
(Angalia huku)
[Beats]
Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa,
Tena ni jambo lenye thamani,
Bali wapumpavu huidharau hekima hii wanahangaika.
Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa,
Tena ni jambo lenye thamaniiii..
Ooh wajinga ndio waliwao
(wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwao mama (wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwaooooo..
Mtu mmoja alilipwa malipo ya uzeeni , akafurahi Sana.
Wakati anarudi nyumbani kwake alikutana na jeshi la Shetani.
Wakamwambia lete pesa tuizalishe, uwe na pesa nyingi
nae pasipo kufikiri kwa Nini hawa wasizalishe zao,
Aliwahesabia pesa zote Matapeli hao wakamwacha pekee
Alisubiri akachoka , mwishowe akagundua
Amekwisha ibiwa
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
[Beats]
Ooh wajinga ndio waliwao
(wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwao mama (wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwaoooo...
Alikuwepo mama mmoja alitafuta dawa,
apendwe na mmewe.
Alileta mizizi hiyo nyumbani
na kumwekea
mmewe kwenye chai.
Tumaini la mama yule mumewe sasa atampenda sana
Laiti Kama angejua kuwa
Upendo
unatoka kwa Yesu
Usiku ulifika Bwana yule akawa tabani
Mpaka akakata roho
Mama yule aligundua kuwa
Haikuwa dawa ,
ilikuwa ni sumu.
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
[Beats]
Ooh wajinga ndio waliwao
(wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwao mama (wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwaoooo..
Mtu mwingine na uzombi wake alinichanganya
Kupigiwa ramli
aliketishwa katika kigoda na elimu take
Akitaka ukubwa
Na kwa kuwa moyoni mwake Yesu hayumo
Hakujua chochote
Laiti Kama angejua
Mganga wake hata shule hakwenda
Alipa pesa kisha akavalishwa ilizi kubwa
Eti apande cheo
Matokeo akafukuzwa kazi siku sio nyingi
Mambo yaligeuka
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Shetani kekundu (kekundu).
[Beats]
Ooh wajinga ndio waliwao
(wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwao mama (wajinga ndio waliwao)
Ooh wajinga ndio waliwaooo...
Binti mmoja Alidhani yakuwa kapata
Kumbe kapatikana
Alikataa wachumba wengi
Waliokuja kuposa
eti ni maskini
Hayawi hayawi yakawa
Alimpata aliyemtafuta
Alimpata mwenye pesa wakaoana
Maisha yakaanza
Vituko vilianza kupishana siku hata siku
Mambo yaligeuka
Dada yule aliona ni afadhali aliyekufa
Asiutese moyo
Kekundu sipende pesa (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kekundu kekundu (kekundu)
Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa
Tena ni jambo lenye thamani
Bali wapumpavu huidharau hekima hii
wanahangaika
Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa
Tena ni jambo lenye thamani