Anthem Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2023
Lyrics
Baba mtoto wako ninayo furaha
Uliyemtuma kanipa uzima
Si mtumwa tena ni huru kabisa
Msalaba asili ya mema
Sikukamilika, kanikamilisha
Sikuwa huru, kaniweka huru
Sikuwa mtoto wake, kaniita mwana
Nilikuwa na dhambi, amenipa haki
Baba wa milele
Upendo wako waniunguza
Baba wa milele
Upendo wako pumzi yangu
(Sikuwa) Sikuwa na maisha kabla
Amenipa uzima wake
Milele
Sikuwa na maisha kabla
Amenipa uzima wake
Milele
Mpango kamilifu wa Mungu kwetu
Tuwe na uzima wake, tusio na hatia mbele zake
Ukamilifu wake ndani yetu watoto wake
Matokeo ya kazi bora kamilifu ya Yesu Bwana wetu
1 Yohana 4:9
Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu,
Kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni
Ili tupate uzima kwa yeye
Sasa sina hatia sina mashitaka
Si laana mimi mbarikiwa
Macho yangu yamefunguliwa
Kiumbe kipya
Sasa sina hatia sina mashitaka
Si laana mimi mbarikiwa
Macho yangu yamefunguliwa
Kiumbe kipya
(Sikukamilika, kanikamilisha) Kanikamilisha
(Sikuwa huru, kaniweka huru) Kaniweka huru
(Sikuwa mtoto wake, kaniita mwana wa pendo lake) Kaniita mwana
(Nilikuwa na dhambi) Amenipa haki
Baba wa milele (Baba wa milele yeah)
Upendo wako waniunguza (Upendo wako wa ajabu)
Baba wa milele (Baba wa milele, eh baba eh baba yeah)
Upendo wako pumzi yangu
(Pumzi yangu yeah, so sikuwa)
Sikuwa na maisha kabla (Na maisha, akaja Yesu)
Amenipa uzima wake (Yeah, ameniokoa)
Sikuwa na maisha kabla (Na maisha, kwa kazi ya msalaba)
Amenipa uzima wake (Wake, sikilizeni furaha yangu)
Sikuwa na maisha kabla (Na maisha, Mungu ni pendo ooh)
Amenipa uzima wake (Wake, sikilizeni habari njema, njema)
Sikuwa na maisha kabla (Huyu baba wa milele, wa milele)
Amenipa uzima wake (Oh yeah)
Amenipa (Bure bure)
Amenipa (Milele yote)
Amenipa (Amani, furaha yake)
Amenipa (Uzima, upendo wake)
Amenipa uzima wake milele (Kaniweka huru, kaniweka huru, nina furaha)
Amenipa amani yake milele (Nina uhakika, yeah, hakuna mwingine angeweza)
Amenipa upendo wake milele (Hakuna mwingine angetoa uhai wake kwa ajili yangu, ahsante kwa upendo wako)
Amenipa uzima wake milele....... (Milele.... Ooh)
Upendo wako waniunguza
Baba wa milele
Upendo wako pumzi yangu
Hakuna hukumu ya adhabu juu ya hao walio katika Kristo Yesu