Boom Focus | Tunamzungumzia Nedy Music
Nedy Music ni miongoni mwa wasanii mahiri wanaosifika kwa nyimbo za mapenzi.
Jina lake kamili, Said Seif Ally na asili yake ni Zanzibar. Anasifika kwa kuimba nyimbo za Afropop, Zouk na Bongo Flava.
Kabla ya kuwa msanii, alikuwa mahiri sana kwenye kucheza yaani dansa, na alitumbuiza kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki kwaajili ya kukuza kipaji chake.
Mwaka 2010 akiwa pamoja na kundi lake, alishiriki kwenye shindano la Dance La Fiesta na kuibuka washindi wa shindano hilo. Mwaka 2011, alishiriki katika shindano la 'Dance Mia Mia' lakini isivyo bahati akashindwa kufika fainali.
Kipaji alichonacho Nedy Music kimetengenezwa kuna kituo mahiri cha kukuza na kulelea vipaji vya muziki maarufu kama Tanzania House Of Talents (THT), ambapo alikaa kwa muda wa mwaka mmoja na kufanikiwa kuhitimu.
Katika kujitafuta kwake kimuziki, Nedy amewahi kufanya kazi chini ya Ommy Dimpoz kupitia lebo ya PKP Entertainment Music Label na kufanikiwa kuachia wimbo wa 'Usiende Mbali' ambao alimshirikisha Ommy Dimpoz na kumfanya taratibu kuanza kutambulika kwenye tasnia ya muziki.
Baada ya hapo rasmi tasnia ikaanza kumtambua na ndipo alipokuja na ngoma yake ya 'Rudi' aliyoiachia mwaka 2016 akimshirikisha mzee wa masauti Christian Bella.
Mpaka sasa, ameshafanikiwa kuachia nyimbo zaidi ya thelathini ambazo zinapatikana rasmi kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki. Miongoni mwa ngoma hizo ni 'Usiende Mbali', 'Rudi', 'Dozee', 'Nishalewa', 'One And Only', 'Homa La Jiji', 'Zungusha', 'Mi Nawe', 'Carino' na nyingine nyingi.
Kwa sasa anatamba na ngoma yake mpya 'Simpi Talaka' ambayo inapatikana Boomplay. Endelea kusikiliza 'Simpi Talaka' hapo chini.
#BuzzBrandColumn #BoomFocus #Music #Trending #NedyMusic
Comments (11)
New Comments(11)
hbmpoleTz
shaa baby 7sf44
nampend xn nedy
joeboymusic
ngoma kali
140887497
nakukubali broo
chrisa de xtopper
nakubali
EUGEN MOLLEL03pgr
hakika
Jizzo Monster
unyamaa mwingi Sana
mrsinia
nedy mkali sana
mrsinia
Namkubar sana nedy music hasa kwa wimbo wake wa "Only you" yaan ni bonge 1 la song kwang
Kidoboyrkyq1
Good historical background
Jofrey chid
vpee
MY BROTHER DAMU YANGU