Boom Discoveries | Mavokali: Staa mpya anayefanya vizuri kwenye game ya muziki
Tasnia ya muziki nchini Tanzania inazidi kukua kwa kasi kadri siku zinavyozidi kwenda mbele.
Kila kukicha wasanii wapya wakali wanazidi kuibuka na kuleta chachu ya kufanya muziki mzuri kwaajili ya kuwapa mashabiki na wapenda muziki kwa ujumla burudani nzuri.
Kwa sasa kuna kijana anaitwa Mavokali ambaye ni moja ya wasanii upcoming wanaofuatiliwa sana kutokana na namna ameupa thamani muziki wake. Ni msanii ambaye ujio wake uliwashtua watu wengi, huku baadhi wakifananisha uimbaji wake na Diamond Platnumz.
Wimbo wake wa kwanza kabisa kumtambulisha ni 'Nitakusahau'. Wimbo huu ni wa mapenzi ambapo Mavokali anazungumzia namna ambayo watu wawili walio kwenye mahusiano hupata shida sana pale wanapoachana na kukumbuka nyakati ambazo walikuwa wakifurahia pamoja.
sasa neno lenye 'Nitakusahau' linakuja pale ambapo kila mmoja kwa waliotengana inabidi wasahau hata pale wanapotembelea maeneno waliyokuwa wakifurahia pamoja ili wapate kuendelea na maisha mengine.
Baada ya ngoma hiyo akaja na 'Yamenizidia', 'Naogopa', 'Dear X', 'Commando' na sasa anatamba na 'Mapopo'.
'Commando' ndiyo ngoma ambayo ilikuja na balaa kubwa sana hususani kwenye mtandao wa TikTok. Ni ngoma ambayo imemfungulia milango mingi sana kuanzia kuitwa kwenye 'shows', kolabo na fursa nyingine mbalimbali.
'Mapopo' ambayo ndiyo ngoma yake mpya kwa sasa ameshirikisha staa mkubwa wa muziki Tanzania, Rayvanny. Endelea kusikiliza 'Mapopo ft Rayvanny' hapo chini kupitia Boomplay.
#BuzzBrandColumn #BoomDiscoveries #Music #Mavokali #Mapopo
Comments (41)
New Comments(41)
Rashid msang
dazzlewwolp
big up
benyjulius196@gmail.com
ubarikiwe na uzur wko
herrynickxous malz
unyama 2 ✊✊
official vanessa
gud
unyama mwingi ngoma kali sana[0x1f628][0x1f636][0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]
merry6njtg
naipenda kazi ako ,,i wish ningekuwa mimi[0x1f641][0x1f638][0x1f604]
Reshmaiwtg5
Hi
140481887
keep it up
moreenkornelio
I love U so much
method philipopdwb1
good
obed kixillos7dkl
big up
shabanrajabu1000@gmail.com
nx
Anajua