Boom Fresh | Ngoma kali zilizoachia wiki na zinapatikana Boomplay hizi hapa
Kila mwisho wa wiki huwa tunakusogezea ngoma ambazo zimeachia wiki nzima kwaajili ya kukukumbusha kusikiliza ngoma hizo endapo utakuwa umepitwa kutokana na shughuli mbalimbali za kila siku.
Wiki hii tumeshuhudia wasanii wakiachia ngoma mbalimbali. Wasanii hao ni Dogo Janja (Pilot), Mimi Mars (Mi Casa Sucasa), Marioo (The Kid You Know), Chege (Chill), Mocco Genius (Nakupenda), Tommy Flavour (Whine 4 Me), Lulu Diva (Nikupe), Billnass (Puuh ft Jay Melody), Christian Bella (Mamelisa).
Pilot ft. GENIUSJINI X66 - Dogo Janja
Msanii wa Bongo Fleva, Dogo Janja amemaliza ukimya wake baada ya kuwashushia mashabiki wake ngoma mpya 'Pilot'. Hii ni ngoma kali ambayo amemshirikisha GENIUSJINI X66. Inawezekana hii ikawa ngoma ya mwisho ya Dogo Janja kwa mwaka huu wa 2022.
Mi Casa Su Casa - Mimi Mars
Mimi Mars amerejea tena kwenye masikio ya wapenda muziki kwa kuachia mkwaju wake mpya Mi Casa Su Casa. Ngoma hii ni ya mapenzi huku jina la ngoma hiyo likiwa limechukuliwa kutoka lugha ya Kispaniola likiwa na maana ya 'Nyumba Yangu Ni Nyumba Yako'. Endelea kuburudika na ngoma hii hapo chini kupitia Boomplay.
The Kid You Know - Marioo
Baada ya kusubiri kwa muda mrefu, hatimaye Marioo ameshusha albamu yake mpya kabisa inayofahamika kwa jina la 'The Kid You Know' yenye jumla ya ngoma 17. Albamu hiyo imejumuisha kolabo za wasanii mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania. Wasanii hao ni Harmonize, Rayvanny, Alikiba, LadiPoe, Tyla, Jux, Fik Fameica na wengine. Ngoma ambazo zilitangulia kuachiwa kabla ya ngoma hii ni My Life, Naogopa, Mi Amor aliyomshirikisha Jovial, na Dear Ex.
Chill ft. Tony Duardo - Chege
Mkongwe kwenye tasnia ya muziki Tanzania, Chege amerudi kusikika kwenye masikio ya wapenda muziki wote kwa kudondosha ngoma yake ya 'Chill'. Ni ngoma ambayo kwa kiasi ina miondoko ya Amapiano. Ni ngoma yake ya nne kwa mwaka huu wa 2022. Endelea kusikiliza ngoma hii hapo chini kupitia Boomplay.
Nakupenda - Mocco Genius
Producer maarufu nchini Tanzania ambaye pia ameamua kufanya muziki, Mocco Genius ameachia ngoma mpya 'Nakupenda'. Ngoma hii yenye maudhui ya mapenzi ya nne kutoka kwake tangu alipoanza kuimba rasmi.
Whine 4 Me - Tommy Flavour
Mkali wa muziki kutoka Kings Music, Tommy Flavour amewabariki wapenda muziki kwa kuwaleta ngoma mpya 'Whine 4 Me' akiwa amemshirikisha Vanillah. Ni wimbo wenye maudhui ya mapenzi. Sikiliza hapo chini kupitia Boomplay
Nikupe - Lulu Diva
Msanii wa muziki, Lulu Diva amewakumbuka mashabiki wake na kuamua kuwapa zawadi ya kuelekea kufunga mwaka baada ya kuachia wimbo mpya 'Nikupe'. Ngoma hii imetayarishwa na FOXXMADEIT.
Puuh ft. Jay Melody - Billnass
Rapa mahiri wa muziki hapa Tanzania, Billnass ameleta wimbo mpya ambao amemshirikisha Jay Melody. Ni ngoma kali ambayo hakika hutapenda kuiruka kwenye playlist yako muda wote. Sikiliza zaidi ngoma hii 'Puuh' hapo chini kupitia Boomplay
#BuzzBrandColumn #BoomFresh #Music #Trending
Comments (2)
New Comments(2)
Gman Kajad Official
marizaka
Nice