Boom Milestone | Ngoma ya Rayvanny 'Nitongoze' imefikisha zaidi ya streams milioni 5 Boomplay
Ngoma ya mpya ya Rayvanny 'Nitongoze' imefanikiwa kufikisha zaidi ya streams milioni 5 kwenye app ya Boomplay.
'Nitongoze' ni ngoma ya Rayvanny ambayo aliiachia Ijumaa, Novemba 11, 2022 na mpaka sasa ni takribani wiki tatu na siku kadhaa zimepita tangu kuachiwa.
Ngoma hii ya Amapiano ambayo amemshirikisha Diamond Platnumz ni moja ya ngoma kali ambazo Rayvanny amefanya na Diamond Platnumz. Ikumbukwe Rayvanny amewahi kuwa chini ya Diamond kupitia lebo ya WCB Wasafi.
Hii inakuwa ngoma ya sita wawili hawa kufanya pamoja. Ngoma nyingine ni 'Vumbi', 'Mwanza', 'Tetema', 'Amaboko', 'Iyena' na 'Salome'.
'Nitongoze' ni ngoma ambayo Rayvanny na Diamond wanasema kuwa jimbo liko wazi na yeyote anayewataka basi ruksa kuwatongoza.
"Hii ni sehemu ya mashairi ya wimbo huu: "Maswali mengi kwa waiter hauna hela nini (Eti), Iyo shingapi hii shingapi hauna hela nini (Eti), Maswali mengi kwa waiter hauna hela nini (Eti), Ile shingapi hii shingapi hauna hela nini, Nimeachwa sitaki tena maswali, Naenda beach kula upepo wa bahari, Naumwagilia moyo mziki kwa mbali, Jimbo likowazi sema nitakubali," Rayvanny.
"Ati unanitaka Eti unanipenda (basi nitongoze) Unanitaka Eti unanipenda (basi nitongoze) Unanitaka
Eti unanipenda (basi nitongoze) Unanitaka Eti unanipenda (basi nitongoze) Eh bwana we," Diamond Platnumz.
Ngoma hii imetayarishwa na moja ya watayarishaji mahiri kwa sasa Tanzania, S2Kizzy. Endelea kusikiliza 'Nitongoze' hapo chini kupitia Boomplay.
Nitongoze ft. Diamond Platnumz
#BuzzBrandColumn #BoomMilestone #Music #Trending #Nitongoze
Comments (38)
New Comments(38)
Emannuel9h79j
nuel FAM
saana
Moudy sogo
Iko pw san
146799282
god bless you
Jamiranga
Hongera
agness1shar
unyama unyama
131401316
udaah mumu
noma sana[0x1f618]
152471553
ni unyama mwaisa
adamm4pan
Unyama mwingi
[0x1f630][0x1f612][0x1f608][0x1f617]