Boom Top | Ngoma kumi kali kati ya 100 ambazo zimefanya vizuri Boomplay wiki hii
Leo ni Jumatatu murua, siku ambayo tunamulika ngoma ambazo zimefanya vizuri ndani ya orodha ya ngoma 100 wiki iliyopita.
Katika kuhakikisha hili linakwenda vizuri, tunakusogezea ngoma 10 ambazo zimeongoza kwenye chati wiki iliyopita.
1. Nitongoze ft. Diamond Platnumz - Rayvanny
Wiki iliyopita staa wa muziki Tanzania, Rayvanny aliachia ngoma mpya 'Nitongoze'. Ngoma hii mpaka sasa imeendelea kufanya vizuri na kufanikiwa kukaa nafasi ya kwanza katika orodha ya ngoma 100 bora Boomplay.
Nitongoze ft. Diamond Platnumz
2. Yataniua ft. Diamond Platnumz - Mbosso
Yataniua ni ngoma ambayo inapatikana kwenye EP mpya ya Mbosso inayojulikana kwa jina la Khan. Ngoma hii yenye mahadhi ya Amapiano ni kali sana na amemshirikisha Diamond Platnumz. Endelea kusikiliza ngoma hii hapo chini.
3. Huyu Hapa
'Huyu Hapa' pia ni ngoma kutoka kwa Mbosso inayopatikana kwenye EP yake ya 'Khan'. Ni ngoma ya kwanza kabisa kwenye EP na ina ladha fulani ya miondoko ya mduara. Inapendeza sana kupigwa kwenye sherehe hususani harusi.
4. Kwikwi - Zuchu
Ngoma hii kutoka kwa Zuchu Kwikwi ni ya Mapenzi ambayo Zuchu anaonesha ni kwa kiasi gani anampenda mpenzi wake huku akimsihi mpenzi wake huyo asimuache kwani anaogopa kuumbuka na kupata aibu mbele za watu.
5. Nidhibiti ft. Zuchu - Jux
Ni ngoma ya Jux ambayo ipo kwenye albamu yake mpya 'King Of Hearts'. Uwepo wa Zuchu kwenye ngoma hii umenogesha zaidi ngoma hii. Endelea kuisikiliza 'Nidhibiti' hapo chini kupitia Boomplay.
6. Champion ft. Nay Wa Mitego - Kontawa
Ngoma hii kali kutoka kwa Kontawa ni kali na inazidi kudhihirisha ubora wake kadri siku zinavyozidi kwenda. 'Champion' ni ngoma fulani ya kutia moyo inayoelezea mapambano ya maisha. Uwepo wa Nay Wa Mitego umezidi kuongeza chachu ya wimbo huu kuwa bora zaidi. Sikiliza ngoma hii hapo chini.
7. Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
Ngoma hii ya Amapiano kutoka kwa Mbosso akiwashirikisha Costa Titch & Alfa Kat inapatikana kwenye albamu yake ya 'Khan'. Ni bonge moja la ngoma ambayo haichoshi kusikiliza muda wote.
Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
8. Cough (Odo) ft. Empire - Kizz Daniel
Baada ya kutamba muda mrefu na ngoma yake Buga (Lo Lo Lo), ngoma nyingine ya Kizz Daniel 'Cough (Odo)' imeanza kutamba kwa kuingia kumi kumi bora ya 100 bora ndani ya app ya Boomplay.
9. Nakupenda - Jay Melody
Ni ngoma kali kutoka kwa Jay Melody huku ikiwa ni miongoni mwa ngoma zinazochezwa sana kwa sasa kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki. Imeendelea kufanya vizuri na kwa sasa imeshika nafasi ya sita kutoka nafasi ya tano wiki iliyopita.
10. Rush - Ayra Starr
Kwa mara ya kwanza, ngoma hii iliingia kumi bora wiki tatu zilizopita. Ni ngoma kali kutoka kwa Ayra Starr ambayo haichoshi kusikiliza. Endelea kusikiliza hapo chini.
Wimbo gani umekuvutia kwenye orodha hii?
#BuzzBrandColumn #BoomTop #Music #Trending
Comments (7)
New Comments(7)
Amayamary
Mcharo zd tito
kali sana
JOHN VENANCExlg4n
Ni kali kinoma nimeikubal
g.lucky06
sem Simba na chui wameuaa xanaaaa ****
haipingwiii hizi boomtop 5[0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]
g.lucky06
haipingwiii hizi boomtop 5[0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]
kilele4real Tz
https://www.boomplaymusic.com/share/playlist/59692076,srModel=COPYLINK&srList=ANDROID
TheNGONIHOODxxiv
bhana hyo top five ni firee ngoma zote kali
Yataniuwa