Boom Discoveries | Kontawa anavyozidi kupaa
Rapa mahiri wa muziki anayekuja kwa kasi, Kontawa ameendelea kuwa gumzo kwenye tasnia ya muziki nchini Tanzania.
Ameendelea kuwa miongoni mwa marapa chipukizi ambao wapenda muziki wameelekeza masikio yao kwaajili ya kuwasikiliza.
Ni kijana ambaye amejipambanua namna ambavyo ameujenga muziki wake na kusikilizwa na kila mtu kutokana na jinsi anavyoyatengeneza maudhui yake.
'Champion Remix' ngoma ambayo amemshirikisha Harmonize inatamba kwa sasa katika vyomba vya habari na majukwaa mengine ya muziki. Mpaka sasa ngoma hii imefikisha streams milioni 1.2 kwenye app ya Boomplay.
Umahiri wa ngoma hii umetokana na jinsi alivyoyasuka maudhui yake na kukubalika na wapenda muziki hususani wale ambao wanaendelea kupambana katika harakati za kusaka maisha bora kila jua linavyochomoza na kuzama.
'Champion Remix ft. Harmonize' inaelezea namna ambavyo mapambano yanavyoanzia chini mpaka mtu kufanikiwa.
Hii ni sehemu ya mashairi ya wimbo huu: Mi nimezaliwa Mtwara Huku ndani ndani Chitoholi Narendele Pengine hata bibi yangu na babu bado wajua rais ni Nyerere Huko kwetu machawa wapo tena wa kikung'ata wanakuwacha na vipele na sio machawa wa mjini hadi mtoto wa kike wanamuonea gere Mi sikumbuki kama Mungu nishamuomba utajiri ila kanipa kwa sababu nastahili....."
Uhodari wa ngoma hii ulitokana na 'Champion' ile ya kwanza aliyofanya na Nay Wa Mitego ambayo kwa sasa ina streams milioni 3.2.
Ngoma hii unaipa asilimia ngapi kwa mashairi yake? Endelea kusikiliza 'Champion Remix ft. Harmonize' hapo chini kupitia Boomplay.
#BuzzBrandColumn #BoomDiscoveries #Music #Kontawa #Champion
Comments (6)
New Comments(6)
Kida Kapole
kisherp0yuz
[0x1f620][0x1f607][0x1f607][0x1f607]
Martha Kimaronl9ou
wow
Deleted User
This comment has been deleted.
ahamadptlid
raeal kontawa anafanya kweli sasa azidi ongeza bidii maana game gumu
Gman Kajad Official
awesome
[0x1f652]