Boom Top | Ngoma 10 kali kati ya 100 bora zilizofanya vizuri Boomplay wiki hii hizi hapa!
Leo ni Jumatatu murua, siku ambayo tunamulika ngoma ambazo zimefanya vizuri ndani ya orodha ya ngoma 100 wiki iliyopita.
Katika kuhakikisha hili linakwenda vizuri, tunakusogezea ngoma 10 ambazo zimeongoza kwenye chati wiki iliyopita.
1. Nitongoze ft. Diamond Platnumz - Rayvanny
Wiki iliyopita staa wa muziki Tanzania, Rayvanny aliachia ngoma mpya 'Nitongoze'. Ngoma hii mpaka sasa imeendelea kufanya vizuri na kufanikiwa kukaa nafasi ya kwanza katika orodha ya ngoma 100 bora Boomplay.
Nitongoze ft. Diamond Platnumz
2. Yataniua ft. Diamond Platnumz - Mbosso
Yataniua ni ngoma ambayo inapatikana kwenye EP mpya ya Mbosso inayojulikana kwa jina la Khan. Ngoma hii yenye mahadhi ya Amapiano ni kali sana na amemshirikisha Diamond Platnumz. Endelea kusikiliza ngoma hii hapo chini.
3. Huyu Hapa
'Huyu Hapa' pia ni ngoma kutoka kwa Mbosso inayopatikana kwenye EP yake ya 'Khan'. Ni ngoma ya kwanza kabisa kwenye EP na ina ladha fulani ya miondoko ya mduara. Inapendeza sana kupigwa kwenye sherehe hususani harusi.
4. Kwikwi - Zuchu
Ngoma hii kutoka kwa Zuchu Kwikwi ni ya Mapenzi ambayo Zuchu anaonesha ni kwa kiasi gani anampenda mpenzi wake huku akimsihi mpenzi wake huyo asimuache kwani anaogopa kuumbuka na kupata aibu mbele za watu.
5. Champion ft. Nay Wa Mitego - Kontawa
Ngoma hii kali kutoka kwa Kontawa ni kali na inazidi kudhihirisha ubora wake kadri siku zinavyozidi kwenda. 'Champion' ni ngoma fulani ya kutia moyo inayoelezea mapambano ya maisha. Uwepo wa Nay Wa Mitego umezidi kuongeza chachu ya wimbo huu kuwa bora zaidi. Sikiliza ngoma hii hapo chini.
6. Cough (Odo) ft. Empire - Kizz Daniel
Baada ya kutamba muda mrefu na ngoma yake Buga (Lo Lo Lo), ngoma nyingine ya Kizz Daniel 'Cough (Odo)' imeanza kutamba kwa kuingia kumi kumi bora ya 100 bora ndani ya app ya Boomplay.
7. Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
Ngoma hii ya Amapiano kutoka kwa Mbosso akiwashirikisha Costa Titch & Alfa Kat inapatikana kwenye albamu yake ya 'Khan'. Ni bonge moja la ngoma ambayo haichoshi kusikiliza muda wote.
Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
8. Nakupenda - Jay Melody
Ni ngoma kali kutoka kwa Jay Melody huku ikiwa ni miongoni mwa ngoma zinazochezwa sana kwa sasa kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki. Imeendelea kufanya vizuri na kwa sasa imeshika nafasi ya sita kutoka nafasi ya tano wiki iliyopita.
9. Champion Remix ft. Harmonize - Kontawa
Baada ya ngoma yake 'Champion' aliyofanya na Nay Wa Mitego kufanya vizuri sana, Champion Remix ft. Harmonize nayo imepokelewa vizuri na hatimaye imeingia kumi bora. Endelea kusikiliza ngoma hii kwa uzuri kabisa kupitia Boomplay hapo chini.
10. Rush - Ayra Starr
Kwa mara ya kwanza, ngoma hii iliingia kumi bora wiki tatu zilizopita. Ni ngoma kali kutoka kwa Ayra Starr ambayo haichoshi kusikiliza. Endelea kusikiliza hapo chini.
Wimbo gani umekuvutia kwenye orodha hii?
#BuzzBrandColumn #BoomTop #Music #Trending
Comments (4)
New Comments(4)
BerryNipeys
rachel4jivk
kiukwel huu wimbo unanifanya najixkia aman pale napokuwa cpo xaw
rachel4jivk
[0x1f627][0x1f627][0x1f627]
rachel4jivk
hii ngoma ni kali xna na ime2lia kixhenz
Cool