Boom Fresh | Ngoma zote zilizoachiwa wiki hii hizi hapa, ngoma gani kali zaidi?
Leo ni Ijumaa ya murua kabisa, siku ambayo huwa tunakusogezea ngoma ambazo zimeachia wiki nzima kwaajili ya kukukumbusha kusikiliza ngoma hizo endapo utakuwa umepitwa kutokana na shughuli mbalimbali za kila siku.
Wiki hii tumeshuhudia wasanii wakiachia ngoma mbalimbali, EP pamoja na albamu. Wasanii hao ni Rayvanny (Unplugged Session EP), Jux (King Of Hearts), Rosa Ree (My Cherie), Meja Kunta (Demu Wangu), Kassim Mganga (Hapa Kati), Mr Blue (Baby Boo), Moni Centrozone (Toto), Kusah (Te Amor), Chin Bees (Ball Remix), Rosa Ree (Goddess), Marioo (My Life),
Unplugged Session - Rayvanny
Rayvanny ameshusha tena kifurushi kipya baada ya kuachia EP yake ya 'Unplugged Session'. Hii inakuwa EP ya nne kwa Rayvanny tangu aanze rasmi kutambulika kwenye muziki. EP nyingine ni 'Vanny Boy', 'Flowers' na 'Flowers II'.
'Unplugged Session EP' ina jumla ya ngoma 8 ambazo ni 'Mzuri', 'I Love You', 'Mtoto', 'Nateswa', 'Mwamba', 'Mama', 'Vacation' pamoja na 'Nipigie'. Kwenye 'Unplugged Session EP', Rayvanny amemshirikisha msanii mmoja pekee ambaye ni Fari by Dar Kid.
King Of Hearts - Jux
Baada ya subira ya muda mrefu, hatimaye staa wa muziki wa R&B nchini Tanzania, Jux ameachia albamu ya 'King Of Hearts' ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki nchini Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.
Katika albamu hiyo yenye jumla ya ngoma 16, imeshuhudiwa Jux akifanya kolabo na wasanii mahiri ndani na nje ya Tanzania kama vile wa Bien kutoka Kenya, Patoranking wa Nigeria, Mbosso wa WCB, Marioo, Zuchu katika ngoma ya 'Nidhibiti' na wakali wengine wengi wa muziki.
My Cherie - Rosa Ree
Rapa mahiri wa kike, Rosa Ree amekuja na ngoma nyingine mpya ambayo inafahamika kwa jina la 'My Cherie'. Hii ni neno linalotokana na lugha ya Kifaransa ambalo linamaanisha 'Mpenzi wangu'. Sikiliza ngoma hii kwa urefu zaidi hapo chini kupitia Boomplay.
Demu Wangu - Meja Kunta
Msanii mahiri wa Singeli, Meja Kunta ameachia wimbo mpya ambao ameupa jina la 'Demu Wangu' akiwashirikisha Mabantu. Kama ilivyo kawaida, Meja Kunta huwa hakosei na hakika kwenye ngoma hii amewapa mashabiki wake kile alichozoea kuwapa, huku uwepo wa Mabantu ukiongeza ladha nyingine.
Hapa Kati - Kassim Mganga ft. AY Masta
Gwiji wa muziki wa kubembeleza kutoka Tanga, Kassim Mganga amewakumbuka mashabiki wake baada ya kuachia ngoma mpya ambayo ameipa jina la 'Hapa Kati' akimshirikisha gwiji mwingine wa muziki Tanzania, AY Masta. Una maoni gani kuhusu ngoma hii?
Baby Boo - Mr Blue
Gwiji wa muziki wa Bongo Fleva, Mr Blue ameachia ngoma mpya ambayo ameipa jina la 'Baby Boo' akiwashirikisha Ibraah & Baddest 47. Ni ngoma kali yenye flow matata ambayo unaweza kuisikiliza Boomplay pekee. Bofya hapo chini kusikiliza 'Baby Boo' kutoka kwa Mr Blue.
Baby Boo ft. Ibraah & Baddest 47
Toto ft. Country Wizzy - Moni Centrozone
Moni Centrozone ameachia dude jipya akimshirikisha Country Wizzy. Ngoma inafahamika kwa jina la 'Toto'. Sikiliza kwa urefu ngoma hii hapo chini kupitia Boomplay.
Te Amor - Kusah
Msanii wa muziki kutoka Tanzania, Kusah ameachia mkwaju mpya 'Te Amor'. Ni ngoma kali ambayo imezidi kuwa tamu zaidi kwa umahiri wa sauti yenye mvuto kutoka kwa Kusah. Isikilize ngoma hii hapo chini.
Ball Remix Chin Bees
Mkali wa trap, Chin Bees ameachia dude jipya 'Ball Remix'. Sikiliza kwa undani hapo chini kupitia Boomplay.
Ball (Remix) ft. William Last KRM
Goddess - Rosa Ree
Mwanadada Rosa Ree amekuja na albamu yake mpya yenye ngoma kali sana ambayo ameipa jina la 'Goddess'. Goddess maana yake ni Mwanamke mahiri. Albamu hii ina jumla ya ngoma 17. Bofya hapo chini kusikiliza albamu nzima.
My Life - Marioo
Siku chache baada ya kufikisha streams milioni 100 Boomplay, Marioo ameachia mkwaju mwingine matata akiupa jina la 'My Life'. Ni ngoma ambayo inazungumzia maisha yake na maisha kwa ujumla. Sikiliza ngoma hii hapo chini kupitia Boomplay.
Ngoma gani imekuvutia zaidi kati ya zote zilizoachiwa wiki hii?
#BuzzBrandColumn #BoomFresh #Music
Comments (32)
New Comments(32)
122398496
122398496
vvvp
jeremiah shamter
hbbp,p,p0,,
tougeousr@gmail.com
Hi
Ronex Kayela
[0x1f60e][0x1f60e]
Chree Jacky
[0x1f605]
ELIA JB
social media Jobs https://eliamwapinga.aweb.page/p/fb08a7e9-2479-47db-9c77-6633d9c7b36a
aminamwela7@gmail.com
mabatu kaua
Vannie Curl
nice[0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]
Memphiso7tja
Ameizng
husna shem
good
neyllanvd82i
very nice♥️♥️♥️
@0682478216