Boom Discoveries | Huyu ndiyo Lody Music, msanii anayeendelea kudhihirisha umahiri wake
Lody Music, ni miongoni mwa majina ya wasanii chipukizi ambao wameendelea kuaminiwa sana mashabiki wa muziki nchini Tanzania.
Lody Music ni moja ya wasanii wa Bongo Fleva ambao wamebahatika kupata idadi kubwa ya mashabiki ndani ya muda mfupi tangu atambulike rasmi.
Tayari amefanikiwa kutoa ngoma nyingi ambazo, si haba zimeedelea kuwa kivutio kwa wapenzi wengi wa muziki kama si wote hususani wale wa nyimbo za mapenzi.
'Kubali' ndiyo wimbo ambao ulimtambulisha kwa ukubwa sana katika tasnia ya muziki nchini Tanzania. Wimbo huu uliipendwa na zaidi ya hapo kuwatoa machozi wale walioonekana kutendwa katika mahusiano yao.
Kama inavyojulikana mapenzi yameteka sehemu kubwa ya maisha ya binadamu, na pengine kila siku watu hupitia maumivu makubwa kutokana na misukosuko mbalimbali inayotokana na mapenzi.
Sasa wimbo wake wa 'Kubali' umeelezea namna ambavyo unapaswa kukubali inapotokea umekumbana na misukosuko ya mapenzi, kwani kama uliyenayo haoni thamani yako basi yuko mtu mwingine nje ya penzi ulilonalo sasa ambaye anaweza kujua thamani yako kwa ukubwa kabisa.
Kuna nyakati kadhaa ambapo wimbo huu umekuwa ukichezwa, huku watu wakijikuta wakidondosha machozi kutokana na maudhui yaliyomo ndani yake.
Mbali na 'Kubali', Lody Music ameachia ngoma nyingine nyingi kama vile 'Naenjoy', 'Hachuji', 'Dear Ex', 'Sweet Love', 'Love Revolution', 'Doreen', 'Promise', 'Only You', 'Vibaya' na nyinginezo.
Mpaka sasa Lody Music amefanikiwa kupata jumla ya streams milioni 10, huku wimbo wa 'Kubali' ukiwa na streams milioni 4.4 na kuwa wimbo ambao umesikilizwa zaidi kati ya nyimbo zake zote zinazopatikana Boomplay.
Nini mtazamo wako kuhusu Lody Music? Endelea kusikiliza ngoma yake ya Kubali hapo chini kupitia Boomplay
#BoomDiscoveries #BuzzBrandColumn #Music #LodyMusic #Trending
Comments (1)
New Comments(1)
teeeee92wkm
huyu jamaa ni super good[0x1f618][0x1f618][0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]