Boom Milestone | Diamond Platnumz afikisha zaidi ya streams milioni 200 Boomplay
Diamond Platnumz anazidi kudhihirisha kuwa ni msanii mkubwa zaidi Afrika Mashariki baada ya kufanikiwa kufikisha zaidi ya streams milioni 200 ndani ya app ya Boomplay.
Anakuwa msanii wa kwanza Afrika Mashariki kufikia mafanikio haya. Kasi ya nyimbo zake kusikilizwa imezidi kuwa kubwa sana Afrika na duniani kwa ujumla. Ikumbukwe alikuwa msanii wa pili Afrika Mashariki kufikisha streams milioni 100 nyuma ya Rayvanny.
Kwa mujibu wa Boomplay, Idadi hii ya streams inaitwa #GoldenClub
Idadi hii ni mchanganyiko wa ngoma zake zote tangu alivyoanza kufanya muziki mpaka sasa ikijumuisha albamu pamoja na EP yake mpya ya 'FOA'.
Wanapotajwa wasanii wakubwa watano barani Afrika kwa sasa, si rahisi jina la Diamond Platnumz kutokuwepo kwenye orodha. Amefanikiwa kutoa ngoma mbalimbali kali zikiwa na kolabo za ndani na nje Tanzania na Afrika kwa jumla. Katika idadi hiyo ya streams ambazo ameipata, kuna ngoma ambazo zimepata streams nyingi zaidi na kuwa chachu ya kufikisha streams milioni 100.
Baadhi ya nyimbo zake ambazo zimempa streams nyingi zaidi ndani ya Boomplay ni 'Gidi' wenye streams 7.1, 'Unachezaje' (streams milioni 4.6), 'Gimmie' (streams milioni 6.9), 'Naanzaje (streams milioni 15.3), 'IYO' (streams milioni 6.2), 'Waah! (streams milioni 6.5) 'Haunisumbui' (streams milioni 6.2) na nyinginezo.
Mbali na ngoma moja moja pia albamu na EP zake zimempa streams nyingi sana. 'First Of All (FOA) mpaka sasa ina streams milioni 78.9, 'A Boy From Tandale ina streams milioni 12.4'. Hii ni kwa uchache tu.
Idadi hii ya streams inamfanya Diamond Platnumz kuungana na baadhi ya wasanii kutoka Nigeria kama vile Burna Boy, Wizikid, Davido, Joeboy, Omah Lay, Fireboy na wengineo.
Project ya mwisho kabisa ya Diamond Platnumz mpaka sasa ni 'First Of All (Acoustic)' ambayo mpaka sasa imefanikiwa kupata streams milioni 2.9 katika app ya Boomplay.
Endelea kusikiliza 'First Of All (Acoustic)' kutoka kwa Diamond Platnumz kupitia Boomplay hapo chini;
#BuzzBrandColumn #BoomMilestone #DiamondPlatnumz #BoomplayGoldenClub
Comments (25)
Top Comments (2)
Mimahcute
hustlerif387
holla at yah boy from Tandale ❤️>
New Comments(25)
saidy prince suddy
WCB nguvu moja
mamumxuvd
ana baya
Ibrahim Munis5x0m6
God bless you
nelson prudence2tq7g
ss tunakulove bigup we pray to you ufanye collable na card b
nelson prudence2tq7g
good god bless you
mammamxy8yr
[0x1f63f][0x1f63f]
mammamxy8yr
simba moto wakukaa nao mbali
mudy babyy6mr1
nakubalii dangote ama ww ni tanzania on
Jah60
big up my brother
Ramadhan Omary2rxsn
hakuna kipingamizi ww kuwa ni moja ya wasanii watajwao ni bora africa na umeshika nafasi hy hongera kaka
Ramseyvo9hu
ana boost huyo hana chchte
Denoz_official
[0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]
sisi tunakupenda sana diamond platnamz kwetu wew ndie dalaja lakufanikiwa unatupa mafunzo nakutuwek imala songa mbele my bro sisi nyuma yako>