Boom Discoveries | Ngoma ya Kontawa 'Champion ft. Nay Wa Mitego' yazidi kufanya vizuri Boomplay
Kontawa, ni miongoni mwa majina ambayo kwa sasa yanasifika kwenye tasnia ya muziki Tanzania.
Ni kijana ambaye amejipambanua namna ambavyo ameujenga muziki wake na kusikilizwa na kila mtu kutokana na jinsi anavyoyatengeneza maudhui yake.
'Champion' ngoma ambayo amemshirikisha Nay Wa Mitego inatamba kwa sasa katika vyomba vya habari na majukwaa mengine ya muziki. Mpaka sasa ngoma hii imefikisha streams milioni 1.5 kwenye app ya Boomplay.
Umahiri wa ngoma hii umetokana na jinsi alivyoyasuka maudhui yake na kukubalika na wapenda muziki hususani wale ambao wanaendelea kupambana katika harakati za kusaka maisha bora kila jua linavyochomoza na kuzama.
'Champion ft. Nay Wa Mitego' inaelezea namna ambavyo mapambano yanavyoanzia chini mpaka mtu kufanikiwa.
Hii ni sehemu ya mashairi ya wimbo huu: "Oya mitaa niliYotoka police wanauza Gongo, Hata uwe mkweli huwezi ishi bila uwongo, Mlo mmoja na bado tulibeba nondo na maisha yakasonga tu eeh Ili sabuni zisiishe tulinyoa madongo, tukala maharage hadi tukacheza juu ya nondo...."
Uhodari wa ngoma hii ukamfanya Kontawa kuachia 'Champion' nyingine akimshirikisha Harmonize.
Ngoma hii unaipa asilimia ngapi kwa mashairi yake? Endelea kusikiliza 'Champion ft. Nay Wa Mitego' hapo chini kupitia Boomplay.
#BuzzBrandColumn #BoomDiscoveries #Music #Kontawa #Champion
Comments (7)
New Comments(7)
jay z official
BerryNipeys
Nice
ommy de OK
oyoo,kontawa naonaumetukumbuka machampion ww na rais wa kitaa..machapion tupooo..
Gman Kajad Official
${href0}
Barton Fredrickrkc0d
Mitaa aliyotoka ni kama mitaa niliyoitokea tumenyoa madongo sana [0x1f602][0x1f602] sema mnyama katishaa kinoma noma[0x1f627][0x1f627][0x1f636][0x1f636] @kontawa # Champion
chadaev9eo
à⁰
kilele4real Tz
mwana anajua sana huyu na ndio wakati wake huu
[0x1f601][0x1f601]