Boom Top | Ngoma 10 zilizofanya vizuri ndani ya 100 bora ya Boomplay wiki hii
Leo ni Jumatatu murua, siku ambayo tunamulika ngoma ambazo zimefanya vizuri ndani ya orodha ya ngoma 100 wiki iliyopita.
Katika kuhakikisha hili linakwenda vizuri, tunakusogezea ngoma 10 ambazo zimeongoza kwenye chati wiki iliyopita.
1. Yataniua ft. Diamond Platnumz - Mbosso
Yataniua ni ngoma ambayo inapatikana kwenye EP mpya ya Mbosso inayojulikana kwa jina la Khan. Ngoma hii yenye mahadhi ya Amapiano ni kali sana na amemshirikisha Diamond Platnumz. Endelea kusikiliza ngoma hii hapo chini.
2. Huyu Hapa
'Huyu Hapa' pia ni ngoma kutoka kwa Mbosso inayopatikana kwenye EP yake ya 'Khan'. Ni ngoma ya kwanza kabisa kwenye EP na ina ladha fulani ya miondoko ya mduara. Inapendeza sana kupigwa kwenye sherehe hususani harusi.
3. Kwikwi - Zuchu
Ngoma hii kutoka kwa Zuchu Kwikwi ni ya Mapenzi ambayo Zuchu anaonesha ni kwa kiasi gani anampenda mpenzi wake huku akimsihi mpenzi wake huyo asimuache kwani anaogopa kuumbuka na kupata aibu mbele za watu.
4. Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
Ngoma hii ya Amapiano kutoka kwa Mbosso akiwashirikisha Costa Titch & Alfa Kat inapatikana kwenye albamu yake ya 'Khan'. Ni bonge moja la ngoma ambayo haichoshi kusikiliza muda wote.
Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
5. Cough (Odo) ft. Empire - Kizz Daniel
Baada ya kutamba muda mrefu na ngoma yake Buga (Lo Lo Lo), ngma nyingine ya Kizz Daniel 'Cough (Odo)' imeanza kutamba kwa kuingia kumi kumi bora ya 100 bora ndani ya app ya Boomplay.
6. Nakupenda - Jay Melody
Ni ngoma kali kutoka kwa Jay Melody huku ikiwa ni miongoni mwa ngoma zinazochezwa sana kwa sasa kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki. Imeendelea kufanya vizuri na kwa sasa imeshika nafasi ya sita kutoka nafasi ya tano wiki iliyopita.
7. Champion ft. Nay Wa Mitego - Kontawa
Ngoma hii kali kutoka kwa Kontawa ni kali na inazidi kudhihirisha ubora wake kadri siku zinavyozidi kwenda. 'Champion' ni ngoma fulani ya kutia moyo inayoelezea mapambano ya maisha. Uwepo wa Nay Wa Mitego umezidi kuongeza chachu ya wimbo huu kuwa bora zaidi. Sikiliza ngoma hii hapo chini.
8. Assalaam ft. Mohammed Almanji - Mbosso
Ni ngoma kutoka kwenye EP ya Mbosso. Ngoma hii imetengenezwa kwa miondoko ya kiarabu na ndiyo sababu ya uwepo wa Mohammed Almanji ambaye amenogesha sana ngoma hii.
9. Rush - Ayra Starr
Kwa mara ya kwanza, ngoma hii iliingia kumi bora wiki tatu zilizopita. Ni ngoma kali kutoka kwa Ayra Starr ambayo haichoshi kusikiliza. Endelea kusikiliza hapo chini.
9. Zuchu - Love ft Adekunle Gold
Ni ngoma mpya na kali kutoka kwa Zuchu ambayo wiki hii imeshika nafasi ya tisa. Ni ngoma kali ya mapenzi ambayo Zuchu amemshirikisha staa kutoka Nigeria, Adekunle Gold.
Wimbo gani umekuvutia kwenye orodha hii?
#BuzzBrandColumn #BoomTop #Music #Trending
Comments (6)
New Comments(6)
Queenpq85m
111981057
[0x1f609][0x1f609][0x1f609]
anko_frankTZ
nice reporting
Isihaka marenda
Og
Neema Chuwatz
[0x1f63f][0x1f63f][0x1f63f]
skizzy boy,tz
skizzy boy
[0x1f641][0x1f641][0x1f641][0x1f641]