Boom Fresh | Ngoma zilizoachiwa wiki hii na zipo Boomplay hizi hapa
Leo ni Ijumaa ya murua kabisa, siku ambayo huwa tunakusogezea ngoma ambazo zimeachia wiki nzima kwaajili ya kukukumbusha kusikiliza ngoma hizo endapo utakuwa umepitwa kutokana na shughuli mbalimbali za kila siku.
Wiki hii tumeshuhudia wasanii wakiachia ngoma mbalimbali. Wasanii hao ni Rayvanny (Nitongoze ft Diamond Platnumz), Young Lunya(Simu), Phina (Hayaa), Paul Clement (Mema), Seneta Worldwide (Nana), Haitham Kim (Ex Mtamu), Malkia Karen (Jinadi), Hamadai (Mususu).
Rayvanny - Nitongoze
Raymond Shaban Mwakyusa, maarufu kama Rayvanny ambaye amewahi kuwa chini ya record label ya WCB Wasafi, amerejea na wimbo mpya unaoitwa 'Nitongoze'. Katika ngoma hii kali, Rayvanny amemshirikisha Diamond Platnumz, ambaye ni staa mkubwa wa muziki Tanzania na Afrika akiongoza lebo ya WCB Wasafi.
'Nikutongoze' ni ngoma yenye vionjo vya muziki wa Amapiano na kwa hakika, Rayvanny ameitendea haki na zaidi uwepo wa Diamond Platnumz umefanya ngoma kuwa bora zaidi.
Nitongoze ft. Diamond Platnumz
Young Lunya - Simu
Msanii wa muziki anayetamba na miondoko ya Trap, Young Lunya amerejea tena kuwapa burudani mashabiki zake kwa kuachia ngoma mpya ya 'Simu'. Hii ni moja ya ngoma kali ambazo Young Lunya amewahi kuachia.
Sikiliza ngoma 'Simu' hapo chini kupitia Boomplay.
Phina - Hayaa
Mwanadada aliyebarikiwa sauti nzuri na ya kuvutia, Phina ameachia wimbo wake mpya ujulikanao kwa jina la 'Hayaa'. Ni ngoma kali ambayo kama ulisikiliza ngoma yake ya 'Nipo Nyonyo' basi huwezi kutofautisha sana.
Inachezeka na ina vibe kubwa sana. Hakika Phina ameendelea kuuthibitishia umma kuwa habahatishi kuanzia kwenye ngoma zake zilizopita.
Seneta Worldwide - Nana
'Nana' ndiyo wimbo mpya kutoka kwa Seneta Worldwide. Ni ngoma nzuri ambayo kwa mtu yeyote mwenye sikio la muziki hawezi kuichukulia poa. Sikiliza 'Nana' hapo chini kupitia Boomplay.
Haitham Kim - Ex Mtamu
Mwanadada mrembo Haitham Kim ameleta ngoma mpya inafahamika kwa jina la 'Ex Mtamu'. Ni wimbo wa mapenzi huu ambao unazungumzia utamu wa mpenzi wa zamani. Sikiliza wimbo huu hapo chini kupitia Boomplay.
Malkia Karen - Jinadi
Malkia Karen amewabariki mashabiki zake na ngoma mpya aliyopipa jina la 'Jinadi'. Ni ngoma yake mpya ambayo ni kama vile anafungia mwaka 2022. Inawezekana akaachia ngoma nyingine lakini 'Jinadi' hakika ni ngoma kali sana akimshirikisha Country Wizzy, mkali wa muziki wa rap.
Hamadai - Mususu
Mkali aliyebarikiwa sauti mahiri sana ya muziki, Hamadai amekuja na ngoma kali 'Masusu'. Sikiliza ngoma hii hapo chini.
Ni ngoma gani imekuvutia zaidi kati ya hizi?
#BuzzBrandColumn #BoomFresh #Music #Trending
Comments (70)
Top Comments (1)
Promise Nov9wp
New Comments(70)
fadhilae22y8
nitongoze[0x1f630][0x1f630]
makdone due Tz
vitamin music
ayubu Chares
damondi
saidp8no9
asssssse hampoi humu
Mtoto Fikirini
❤❤❤❤❤simu
Irene Urban
nitongoze [0x1f618][0x1f618]
ayubu Chares
come
ayubu Chares
reivan
japhet onesimo6ee48
simu from young lunya
zebidap0iln
nitongoze by rayvanny
Mzukivanny007
Simu
Erick Mrossoeq2k0
vannny bwayyyy
sim >