Boom Focus | Tunamtaza Young Lunya
Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimejaaliwa wasanii wengi wenye vipaji vikubwa vya kuimba, kurap na kadhalika. Tangu enzi za wakongwe kina Marijan Rajab, Mbaraka Mwinshehe, Hemed Maneti mpaka kizazi cha sasa, bado wanauwasha moto vilivyo.
Kwenye miondoko ya Hip Hop kumekuwa na wasanii bora kizazi na kizazi. Tumeshuhudia kizazi cha kina Joseph Mbilinyi 'Mr II' au Sugu, Professor J, Mwana FA, AY, Fid, Mr Blue, Chidi Benz na wengine wengi.
Kumeibuka tena kizazi kingine cha kina Country Boy, Young Killer, Young Lunya na wengine kadha wa kadha. Na leo tumemzungumzia Young Lunya.
Pamoja na kuwa na marapa wakali wengi kwenye kizazi cha sasa, rapa Young Lunya ameonesha kuna kitu anacho. Huyu ni msanii ambaye kipaji chake kilianza kunawiri tangu wakati yuko kwenye kundi la OMG ambalo lilikuwa likiuundwa na wasanii watatu ambao ni Salmin Swaggz, Conboi na Young Lunya mwenyewe.
Umahiri wake ukajizidi kudhihirika zaidi baada ya kuanza kutoa kazi zake kama 'Solo Artist'. Young Lunya ana flows, skills, punch na kadhalika. Zaidi ya hapo ni mwandishi mzuri na pia anaweza kuimba ka umahiri wa hali ya juu sana.
Ingawa bado ana mengi zaidi ya kuendelea kuthibitisha kwa umma, bado si vibaya kumpa sifa zake ili azidi kuimarika kadri siku zinavyozidi kwenda na baadaye aje kuwa moja ya magwiji wa muziki. Kuna baadhi ya watu wameshawahi kudiriki kumfananisha na wakali kama Meek Mill au T.I yule wa Live Your Life au mtu mzima Kendrick Lamar na albamu yake ya DNA.
Tayari ameshafanya ngoma kadhaa kali na nyingine akishirikishwa na kufanya vizuri sana. Ngoma ambazo mpaka amefanya ni Tikisa, Freestye session 1, 2 na 3, Mbuzi, Fimbo, Announcement, Moto na nyinginezo.
Kwa sasa Young Lunya yuko chini ya lebo kubwa ya muziki ya Sony Music Entertainment akisimamiwa kazi zake kwa viwango vya juu kabisa. Young Lunya ni miongoni mwa wasanii wanaoakisi mapambano halisi kuanzia 'hamna kitu mpaka kuwa na kitu'.
Sikiliza ngoma yake 'Vitu Vingi' ambayo ndiyo ya mwisho kuachia mpaka sasa.
Nini mtazamo wako kuhusu rapa huyu?
#BuzzBrandColumn #BoomFocus #Music #Trending #YoungLunya
Comments (34)
New Comments(34)
zerah hussy
Ghanty Akouèwa
Ghanty Akouèwa
Testimony of Master Mr Ganty Akouèwa :+229 56 02 05 91 The truth is dûre to believe nowadays but I advise you for everything is worth the problem of life ☻, households, work where health return of affection even to multiply your money ↩️ justice problem. WhatsApp : +229 56 02 05 91
Joshua Jacobgfp0w
naqubal sana [0x1f630][0x1f630]
johanes kipande
iko waz mbuz anajua
brownr28hw
anajuh san uyu jamaa
Young Teflon P1 9th
wa motrooo ...! [0x2600][0x26a1] ... [0x1f60d]
Izsack Enock
rap trap boy
khanamaneno@gmail.com
cmkubal huyu hata chembe
Manray George
Oooh my[0x1f41c]
mwandembwejoseph
namkubaki .mwamba uyo
sancho jn
unamkubalu aucio
mh na mkubalu sana young lunya
namkuali sana rapper young lunya ni moto wa kuotea mbali [0x1f630]