Boom Discoveries | Tunamtaza Vanillah kutoka Kings Music
Vanillah ndiyo jina ambalo linatamba kwa sasa miongoni mwa wasanii wanaochipukia katika tasnia ya muziki nchini Tanzania.
Huyu ni msanii mpya ambaye hivi karibuni alitangazwa kusainiwa na lebo ya Kings Music iliyopo chini ya gwiji wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba.
Ujio wake umeshtua watu wengi kutokana na kuanza kwa kishindo kikubwa baada ya kuachia EP yake inayofahamika kwa jina la 'Listen To Me' yenye jumla ya ngoma sita za moto. Historia ya Vanillah ambaye jina lake halisi ni Fanuel Fabian Peter imeanzia jijini Mwanza ambapo ndipo alipozaliwa, kukulia na kuanza harakati zote za muziki.
Safari yake ya muziki ilianza mwaka 2012 wakati akiwa shuleni ambapo alikuwa akiimba cover za nyimbo za wasanii mbalimbali na baada ya kumaliza shule akaanza kupambana rasmi kufanya ngoma zake mwenye na hatimaye kufanikiwa kutoa ngoma yake ya kwanza kabisa akiwa msanii anayejitegemea mwaka 2019.
Baadaye aliamua kufanya safari ya kwenda Dar es Salaam kwaajili ya kupanua fursa zaidi na ndipo safari yake ya kujiunga na Kings Music ilipoanzia baada ya mtayarishaji mahiri na maarufu Yogo Beats ambaye alikuwa akifanya naye kazi kuvutiwa na kumpeleka kwa Alikiba kushiriki katika moja ya ngoma zake zilizopo kwenye albamu ya Only One King.
Ngoma ambayo alishiriki kuiandaa ni 'UTU' ambayo ndiyo ngoma pendwa zaidi kwenye albamu ya Only One King ya Alikiba.
Kwa sasa EP ya Vanillah 'Listen To Me' imefanikiwa kufikisha zaidi ya streams 200k kwenye app ya Boomplay. Endelea kusikiliza 'Listen To Me' ya Vanillah hapo chini kupitia Boomplay.
#BuzzBrandColumn #BoomDiscoveries #Music #Vanillah #ListenToMe
Comments (3)
New Comments(3)
nelo bvr5zj
Musa Mgalla
janja yuko poa sana namsapoti akaze tu mziki wa saivi siyo simpo sana kama nyuma au zaman
Johnbaba255
sounds good
anaupiga mwingi japo promotion kwnye rebo yake ipo chini sana