Boom Top | Hizi ndizo ngoma kali 10 ambazo zimetamba Boomplay wiki iliyopita
Leo ni Jumatatu murua, siku ambayo tunamulika ngoma ambazo zimefanya vizuri ndani ya orodha ya ngoma 100 wiki iliyopita.
Katika kuhakikisha hili linakwenda vizuri, tunakusogezea ngoma 10 ambazo zimeongoza kwenye chati wiki iliyopita.
1. Yataniua ft. Diamond Platnumz - Mbosso
Yataniua ni ngoma ambayo inapatikana kwenye EP mpya ya Mbosso inayojulikana kwa jina la Khan. Ngoma hii yenye mahadhi ya Amapiano ni kali sana na amemshirikisha Diamond Platnumz.
2. Huyu Hapa
'Huyu Hapa' pia ni ngoma kutoka kwa Mbosso inayopatikana kwenye EP yake ya 'Khan'. Ni ngoma ya kwanza kabisa kwenye EP na ina ladha fulani ya miondoko ya mduara. Inapendeza sana kupigwa kwenye sherehe hususani harusi.
3. Kwikwi - Zuchu
Ngoma hii kutoka kwa Zuchu Kwikwi ni ya Mapenzi ambayo Zuchu anaonesha ni kwa kiasi gani anampenda mpenzi wake huku akimsihi mpenzi wake huyo asimuache kwani anaogopa kuumbuka na kupata aibu mbele za watu.
4. Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
Ngoma hii ya Amapioano kutoka kwa Mbosso akiwashirikisha Costa Titch & Alfa Kat inapatikana kwenye albamu yake ya 'Khan'. Ni bonge moja la ngoma ambayo haichoshi kusikiliza muda wote.
Shetani ft. Costa Titch & Alfa Kat
5. Nakupenda - Jay Melody
Ni ngoma kali kutoka kwa Jay Melody huku ikiwa ni miongoni mwa ngoma zinazochezwa sana kwa sasa kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki. Imeendelea kufanya vizuri na kwa sasa imeshika nafasi ya tano kutoka nafasi ya pili wiki iliyopita.
6. Cough (Odo) ft. Empire - Kizz Daniel
Baada ya kutamba muda mrefu na ngoma yake Buga (Lo Lo Lo), ngma nyingine ya Kizz Daniel 'Cough (Odo)' imeanza kutamba kwa kuingia kumi kumi bora ya 100 bora ndani ya app ya Boomplay.
7. Assalaam ft. Mohammed Almanji
Ni ngoma kutoka kwenye EP ya Mbosso. Ngoma hii imetengenezwa kwa miondoko ya kiarabu na ndiyo sababu ya uwepo wa Mohammed Almanji ambaye amenogesha sana ngoma hii.
8. Pole ft. Ruby
Ngoma hii ambayo amemshirikisha mwanadada mahiri na mwenye sauti ya kipekee, Ruby imefanikiwa kushika nafasi ya nane. Hii ni moja ya ngoma kali kutoka kwenye albamu hii.
9. Zuchu - Love ft Adekunle Gold
Ni ngoma mpya na kali kutoka kwa Zuchu ambayo wiki hii imeshika nafasi ya tisa. Ni ngoma kali ya mapenzi ambayo Zuchu amemshirikisha staa kutoka Nigeria, Adekunle Gold.
7. Rush - Ayra Starr
Kwa mara ya kwanza, ngoma hii iliingia kumi bora wiki tatu zilizopita. Ni ngoma kali kutoka kwa Ayra Starr ambayo haichoshi kusikiliza. Endelea kusikiliza hapo chini.
Wimbo gani umekuvutia kwenye orodha hii?
#BuzzBrandColumn #BoomTop #Music #Trending
Comments (47)
New Comments(47)
Godfrey Daudignarj
Ester Johnzwt9y
mbosso utaua watuu jamn mbosso
hii boomplay ya mboss
@DeejayToxic3
Hii COUGH ya Kizz Daniel imekuwa tishio kubwa mtaani
Ibrahim Felixe32ue
ibrahimfelix46@gmail.com namkubali mbosso na mondi
diraxjwayj
mbona konde ayupo jamn
totoo2ugx2
♥️
fredy14
iko vere
Veronica Buyanza
wote wakarii
masalu1f3b6
music
laxy lee
ngoma kali xanaaah
Happy Haroun
Sawa
Ni shida